Wasaidie Wenye Mioyo Yenye Ufuataji Haki Watoroke Babuloni Mkubwa
1 Onyo kali lililorekodiwa katika Ufunuo 18:4 limekuwa lenye uharaka zaidi kwa sababu ya nyakati zetu. Mashaka yoyote kuhusu utambulisho wa kweli wa Babuloni Mkubwa yameondolewa. Amefunuliwa waziwazi kuwa milki ya ulimwengu ya dini bandia inayotumiwa na Shetani kupigana dhidi ya uzao wa “mwanamke” wa Mungu.
2 Kubaki ndani yake kunamfanya mtu ashiriki dhambi zake. Hata hivyo, mengi yanahitajiwa zaidi ya kuacha dini bandia tu. Hakuna mtu anayeweza kuwa mwenye ubaridi kuhusu ibada ya kweli na bado atazamie kupokea baraka za Yehova. Wale wanaokimbia Babuloni lazima wajifunze Neno la Mungu, wajiunge katika kupiga mbiu ya habari njema, na wawe watumishi wa Mungu waliojiweka wakfu na kubatizwa.
3 Je! wote ambao walihudhuria Ukumbusho Machi 22 wanahisi uharaka wa kutoka katika Babuloni na kuwa watumishi wa Yehova waliojiweka wakfu kabisa. Lazima tuwasaidie wowote ambao wanasitasita wachukue msimamo wao upande wa Yehova. (Yak. 1:8; 4:8) Fanya jitihada ya pekee kuwapa matoleo ya Aprili na Mei ya Mnara wa Mlinzi. Wasaidie wathamini kwamba kwa kuwa wakati uliobaki umepunguzwa, kuna uhitaji wa haraka wa kuchukua msimamo wao sasa.—Mt. 12:30.
WASAIDIE WAPYA
4 Tukiwa tunakumbuka vizuri sana mwadhimisho wa Ukumbusho, kulingana na akili nzuri Aprili ni wakati wa kuwasaidia wapya wang’amue kwamba kushiriki huduma ya shambani ni njia bora ya kuonyesha kwamba wanastahi dhabihu ya Yesu kwa njia inayofaa. Ndiyo, ni njia inayohitajiwa sana kuonyesha jinsi tunavyothamini yale ambayo Yehova na Mwana wake, Yesu, wametufanyia!
5 Je! unaongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani ukiwa na kusudi la kuwatayarisha wanafunzi wapya kwa ajili ya huduma ya shambani? Wanahitaji msaada wa hatua kwa hatua na kitia-moyo ili wakuze uthamini kwa daraka hili la Kikristo. Waeleze wanafunzi wako umuhimu wa utumishi wa shambani, na uonyeshe jinsi unavyofanywa. Utaona ya kuwa broshua Wanafanya Mapenzi ya Mungu ni yenye msaada kwa habari hii.
KUTIMIZA MATAKWA
6 Wakati mwanafunzi wa Biblia amefanya maendeleo thabiti na anaonyesha tamaa ya kusaidia kutimiza Mathayo 24:14, lingekuwa jambo lenye mafaa kupitia yale ambayo yametaarifiwa kwenye kurasa 98 na 99 za kitabu Huduma Yetu. Anapasa kuwa na uwezo wa kustahili ‘kutumia kwa halali neno la kweli.’ (2 Tim. 2:15) Usimwalike aandamane nawe katika utumishi wa shambani kwa mara ya kwanza mpaka wazee watoe idhini ya kushiriki kwake. Ikiwa kwako inaonekana kwamba ametimiza matakwa ya Kimaandiko na kitengenezo, acha mwangalizi msimamizi ajue kuhusu maendeleo yake. Ikiwa wazee wanakutana na mmoja wa wanafunzi wako wa Biblia katika Aprili na kutoa idhini ashiriki utumishi wa shambani, mfunze jinsi ya kutoa uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi, na anza kumzoeza katika huduma ya nyumba kwa nyumba.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Novemba 15, 1988, kurasa 16-17, mafungu 7-10.
7 Babuloni Mkubwa anaelekeana na uharibifu kamili! Kabla huo haujatokea, tunahitaji kuwasaidia wenye mioyo ya ufuataji haki watoroke nguvu zake na kuja katika tengenezo la Yehova. Tayari mamilioni wamesaidiwa wafanye hivi. Ikiwa ni mapenzi ya Yehova, wengi zaidi wanaweza kusaidiwa wakimbie kutoka miongoni mwa Babuloni anapobariki jitihada yetu yenye bidii ya kupata na kutunza wenye mioyo ya ufuataji haki katika eneo letu.—Yer. 50:8.