Kupanga Kimbele kwa Ajili ya Septemba
1 Kwa kutazamia mwanzo wa mwaka mpya wa utumishi katika Septemba, ni vema kwa wote wanaopendezwa na utumishi wa Ufalme wafikirie yale ambayo tumetimiza kufikia sasa na yale ambayo tunataka kutimiza katika mwaka ulio mbele. Kama alivyosema mtume Paulo: “Kwa kadiri tulivyofanya maendeleo, na tuendelee kutembea kwa utaratibu katika kawaida ii hii.”—Flp. 3:16, NW.
2 Septemba unamaanisha mwisho wa kipindi cha pumziko kwa wengi walio na umri wa kwenda shule. Kwa hiyo kwa nini msitumie mwisho-juma wa kwanza ili mfanye kazi pamoja na mapainia katika kundi lenu na kuanza vizuri katika utumishi kwa ajili ya mwaka mpya wa utumishi? Vijana fulani wamefanya mradi wao uwe kuwatolea ushuhuda zaidi wanafunzi wenzake na kujaribu kuanzisha funzo la Biblia. Au kwa wale kati yenu ambao ni wazazi na ambao watoto wao wataenda shuleni, je! huenda huu ukawa mwezi mzuri wa kushangilia kazi ya upainia msaidizi tena? Mtakuwa na Jumamosi moja zaidi katika mwezi ili iwasaidie mtimize matakwa.
3 Kwa vijana wahubiri, muhula wa shule mara nyingi hutokeza mgawo wa kufanyia nyumbani. Je! mtaratibu wakati kwa ajili ya funzo la kitheokrasi na pia mgawo wenu wa kufanyia nyumbani? Kutawasaidia mstahili kwa ajili ya kazi-maisha katika utumishi wa wakati wote na kuwasaidia mkae kwenye barabara ya uhai. (Isa. 30:21) Nyakati fulani tunahisi tukiwa na shughuli sana tusiweze kufanya zaidi. Lakini wakati wenye thamani unaweza kupotezwa kwa kutazama televisheni. Mbona msitumie wakati huo katika mambo ya kutangulizwa ya kitheokrasi?—1 Tim. 4:15.
4 Msiache saa au miezi ipite kama mawingu katika anga, bali, pangeni wakati wenu na mweke miradi ili mtumie uhai wenu katika njia ambayo itamletea Yehova sifa.—Mhu. 11:4.