Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/89 kur. 1-2
  • Kupata Shangwe Kupitia Maangusho ya Magazeti Yaliyoongezeka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kupata Shangwe Kupitia Maangusho ya Magazeti Yaliyoongezeka
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MFIKIO CHANYA
  • Weka Kando Wakati kwa Ajili ya Utendaji wa Magazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Toa Magazeti Katika Huduma
    Huduma ya Ufalme—2005
  • ‘Kupanda kwa Kusudi la Ukweli’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 9/89 kur. 1-2

Kupata Shangwe Kupitia Maangusho ya Magazeti Yaliyoongezeka

1 Tengenezo la Yehova la ulimwengu wote mzima lajulikana kwa utokezaji walo wa mazao. Kwa njia ya Yesu Kristo, Yehova amesitawisha tengenezo la kidunia ambalo pia lina sifa ya kuwa na wafanya kazi wenye kutokeza mazao kwa moyo wa kupenda. (Zab. 110:3; Mt. 9:37, 38) Tunapotoa uangalifu kwa ubora pamoja na kiasi cha huduma yetu, shangwe iliyoongezeka itatokea hakika. (Luka 10:17) Hasa hiyo ni kweli tukazapo akili zetu kwa ajili ya kuongeza ugawanyaji wetu binafsi wa magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

2 Ugawanyaji wa magazeti ndiyo mojapo njia kuu ambazo katika hizo ujumbe wa Ufalme huenezwa kotekote. Ingawa hiyo yaendelea kuwa kweli kadiri kazi ya kuhubiri ipanukavyo, imeonekana kwamba katika maeneo fulani maangusho yanapungua. Mwelekeo huo waweza kuponeshwaje? Ni nini baadhi ya mambo ya lazima tunayoweza kuweka akilini ambayo yatatusaidia sisi binafsi kuangusha magazeti zaidi?

MFIKIO CHANYA

3 Hatua ya kwanza kuelekea maangusho yaliyoongezeka ni: FAHAMU MAGAZETI. Lengo hilo linafikiwa kwa urahisi wakati sisi wenyewe tunapokuwa wasomaji wa kawaida wa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mara tunapofahamiana na yaliyomo, tunataka kutumia kila pindi inayofaa kuyatoa kwa watu wote. Kwa walio wengi wetu, kila Jumamosi hutoa fursa nzuri kushiriki katika kugawanya magazeti nyumba kwa nyumba. Makundi mengi hutenga wakati kwa ajili ya utendaji wa magazeti wa katikati ya juma ili kuwatia ndani wahubiri ambao hawawezi kufanya kazi katika utumishi wa shambani Jumamosi. Huenda wengine wakaona kwamba kutoa ushahidi jioni hutoa fursa nzuri za kutoa magazeti nyumba kwa nyumba. Utendaji wa duka kwa duka, kutoa ushahidi vivi hivi, na kupelekea watu magazeti kwa ukawaida zote ni njia nzuri ambazo katika hizo sisi tunaweza kushiriki kugawanya magazeti. Katika kazi ya kawaida ya nyumba kwa nyumba, magazeti ya karibuni zaidi yaweza kutolewa wakati toleo la wakati huo la mwezi linapokataliwa. Kuwa chonjo kufanya hivyo kwaweza kuongeza shangwe yetu.

4 Dokezo la pili kwa ajili ya kuongeza maangusho ya magazeti ni: IFANYE IWE RAHISI. Kwa wazi baadhi ya wahubiri wanaongea sana na kujizuia kuangusha magazeti kwa kutoa mahubiri marefu. Wahubiri wengine wanatumia Kichwa cha Mazungumzo wanaposhiriki kazi ya magazeti. Hata hivyo, hilo halipendekezwi. Ulipokuwa ukitia moyo ugawanyaji wa magazeti ulio mpana zaidi, Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1956 (Kiingereza), ulitaarifu hivi: “Utoaji mfupi wenye kusema mambo wazi ndio bora zaidi wakati wa kutoa magazeti. Lengo ni kuangusha nakala nyingi. Hizo ‘zitajisemea’ zenyewe. Sosaiti inadokeza utoaji wa nusu dakika kufika dakika moja, taarifa yenye maneno yaliyochaguliwa vizuri ya jambo moja linalozungumziwa katika gazeti linalotolewa.”

5 Halafu: UWE MWENYE KUBADILIKANA. Tayarisha utoaji zaidi ya mmoja. Ndipo unapokutana na hali tofauti-tofauti, utaweza kunena na watu wa namna zote na kupatanisha utoaji wako na mapendezi yao. Kutanguliza kujitayarisha hivyo huongoza mara nyingi kwenye ugawanyaji ulioongezeka wa magazeti na shangwe kubwa zaidi.

6 Dokezo moja la mwisho: WEKA MRADI WA KIBINAFSI. Huenda ukakumbuka kwamba hilo lilikaziwa katika nyongeza “Magazeti Yaonyesha Njia Inayoelekeza Kwenye Uzima,” iliyotokea katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Aprili 1984. Huenda ukataka kujitahidi kupata wastani wa gazeti moja kwa kila saa unapokuwa katika utumishi kwa kila mwezi. Mradi wako wa kibinafsi wapaswa uwe wa kiasi, kwa kufikiria hali zako binafsi na wakati unaoweza kutumia katika utumishi wa shambani.

7 Kwa njia ya tengenezo lake lionekanalo, Yehova huendelea kuandaa tunayohitaji kuongeza ushiriki wetu katika huduma. Sisi tuna magazeti ya kusisimua yenye rangi ya kufanya kazi nayo. Sasa ushirikiano wetu sisi mmoja mmoja pamoja na mipango ya kundi kwa ajili ya kugawanya magaeti unahusika. Kwa kuwa utendaji huo humtukuza Yehova, sisi tutapata shangwe yenye kina kirefu inayotokana na ushiriki ulioongezeka katika huduma kwa magazeti.—Yoh. 15:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki