Saidia Wengine Wathamini Muumba Wetu Mtukufu
1 Tutazamapo uumbaji unaotuzunguka, hakuna shaka katika akili zetu kwamba Muumba yuko na kwamba yeye anapendezwa sana na wakati wetu ujao. (Rum. 1:20) Kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? kimesaidia sana kunoa uthamini wetu kwa ajili ya Muumba. Kimesaidia pia kuwaeleza wengine jinsi uhai ulipata kuwako.
2 Baada ya kusoma kitabu hicho, mtu mmoja mwenye malezi ya kisayansi alikieleza kuwa ndicho kitabu bora zaidi ambacho amepata kusoma cha kujenga uthamini kwa ajili ya uhai. Profesa mmoja wa koleji alitaarifu hivi: “Sijapata kamwe kuona hoja iliyotolewa vizuri hivyo kuunga mkono uumbaji.” Kwa wazi, kitabu Creation kimekuwa chombo kizuri katika kusaidia wengi wathamini Yehova Mungu, Muumba wetu Mtukufu.
TUMIA KWA FAIDA FURSA ZOTE ZINAZOFAA
3 Wakati wa mwezi wa Septemba, tunaweza kutumia kitabu hiki kikiwa toleo la badala katika huduma ya shambani. Kuongezea huduma yetu ya kawaida ya nyumba kwa nyumba, tunaweza kutoa kitabu Creation tunapotoa ushahidi wa vivi hivi. Tunaweza kukitoa kwa wafanya kazi wenzi, wanashule wenzi, watu wa ukoo, na wengine tunaoonana nao. Je! wanafunzi wako wa Biblia wanacho? Ikiwa sivyo, sababu gani usihakikishe kwamba wanapata kimoja? Je! wewe una watu unaopelekea magazeti kwa ukawaida? Huenda ikawa kwamba watu hao wangependa kuwa na nakala moja. Tumia kwa faida kila pindi inayofaa kutoa kitabu Creation.
4 Wengi walio wachanga wamekuwa na mafanikio katika kuangusha kitabu Creation shuleni. Je! wewe umejaribu kuchukua nakala moja uende nayo shuleni? Wakati wale wenye udadisi wanapokuuliza maswali, utakuwa na fursa ya kuwatolea ushahidi.
KICHWA CHA MAZUNGUMZO KILICHO BADALA
5 Toleo la kitabu Creation hupatana vizuri na kile Kichwa cha Mazungumzo “Abudu Mpaji Uhai.” Katika kutoa kitabu hicho, waweza kusema: “Watu wengi wanapendezwa kujua jinsi uhai ulivyoanza. Je! wewe umepata kutaka kujua hilo? [Ruhusu itikio.] Kuna maoni mbalimbali juu ya asili ya uhai. Acha tuzungumzie elezo la Biblia lenye kupatana na akili. [Soma Waebrania 3:4.] Hivyo kupatana na kufikiri kuzuri kila jengo au nyumba tunayoona kutuzunguka leo ilikuwa na mbuni na mjenzi. Kwa wazi, ulimwengu wote mzima ambao ni tata zaidi lazima uwe ulikuwa na muumba. Kulingana na Waebrania 3:4, Muumba huyo ni Mungu. Lakini maarifa ya kujua hivyo yapasa yatuathirije? [Soma Ufunuo 4:11.] Kwa hiyo mwendo wa hekima kuchukua wakati kungali na wakati ni kujifunza mapenzi ya Muumba na kupatanisha maisha yetu nayo.” Ndipo utoe kitabu, ukitaja kwamba kitaonyesha jinsi mwanadamu alivyopata kuwa hapa na jinsi utii kwa Muumba wetu unavyoweza kuongoza kwenye uhai wa milele.
6 Sisi tunafurahi kama nini kuwa na buku hili la kurasa 256 lenye vielezi vizuri sana ambalo hueleza ukweli juu ya mageuzi na juu ya uumbaji! Hata hivyo, kwanza kabisa kitabu hiki humheshimu Muumba wetu Mtukufu. Kinafanya hivyo kwa kutujulisha jinsi uhai ulivyopata kuwa hapa, kusudi zuri ajabu la Yehova la kutakasa jina lake, na ahadi yake ya kubariki aina ya binadamu kupitia Ufalme.