Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/92 uku. 8
  • Utoaji Mbalimbali Unaochochea Kupendezwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utoaji Mbalimbali Unaochochea Kupendezwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwasaidia Wengine Wamheshimu Mfanyi Wetu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Kujenga Imani Katika Muumba wa Wanadamu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Saidia Wengine Wathamini Muumba Wetu Mtukufu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Kitabu Creation
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 9/92 uku. 8

Utoaji Mbalimbali Unaochochea Kupendezwa

1 Tunapaswa nyakati zote kuonyesha kupendezwa kibinafsi kwa uchangamfu na watu tunaokutana nao katika huduma ya shambani. Kuwauliza maoni yao juu ya mambo huonyesha staha yetu kwa maoni yao. Huenda habari tunayotoa na maswali tunayouliza yakachochea fikira zao na kuwafanya watake kujifunza zaidi kuhusu Mungu na makusudi yake kwa ainabinadamu.

2 Wakati wa Septemba tutakuwa tukielekezea fikira ukweli kuhusu uumbaji tunapotoa kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? kwa wale wanaosema Kiingereza au Kifaransa. Chukua wakati wewe binafsi kupitia kichapo hicho, na uteue mambo hususa utakayokazia. Unapozungumzia habari katika kitabu Creation, kifungue na umpe mwenye nyumba. Rejezea habari na vielezi hususa. Uwe mchangamfu unapoonyesha thamani ya kichapo hicho chenye kuvutia.

3 Baada ya kujijulisha kwa uchangamfu, ungeweza kusema:

◼ “Katika ulimwengu huu wa ki-siku-hizi na wa kisayansi, je! ni jambo la akili kuamini kuna Mungu aliyetuumba pamoja na dunia hii yenye kupendeza ambayo twaishi juu yayo? [Ruhusu itikio.] Tunapofikiria ukubwa na maajabu ya dunia na ulimwengu wote mzima, tunavutiwa na utaratibu na jinsi ilivyobuniwa. Je! hiyo haitoi ushuhuda wa kuwapo kwa Muumba? Angalia mawazo ya Biblia kuhusu jambo hilo. [Soma Waebrania 3:4.] Kupatana na akili nzuri, kila jengo lilikuwa na mbuni na mjenzi walo. [Toa kitabu Creation na ufungue kwenye kielezi katika ukurasa 114.] Ulimwengu wetu mzima ni wenye kuhofisha! Je! unafikiri ungejitokeza wenyewe?” Halafu fungua ukurasa 122 na usome maelezo yaliyo chini ya picha ya saa. Kielezi na andiko lililonukuliwa katika ukurasa 127 yaweza kutumiwa pia. Mambo zaidi yenye kusaidia yaweza kupatikana katika kitabu Kutoa Sababu, kurasa 397-401.

4 Au huenda ukasema:

◼ “Unafikiri ni nini kinachotakiwa ili ainabinadamu ipate amani na furaha ya kweli duniani? [Ruhusu itikio.] Biblia husema kwamba ni lazima tumhofu Mungu na kumkiri yeye kuwa Muumba wa mbingu na dunia.” Soma Ufunuo 14:7, halafu ufungue kitabu Creation kwenye kurasa 140 na 141, labda ukisoma mafungu 24 na 25, mahali panapoeleza kwamba dunia imebuniwa ili ikaliwe na mwanadamu. Ikiwa mwenye nyumba anapendezwa sana na unataka kuendelea na mazungumzo, fungua sura ya 19 na ueleze jinsi paradiso ya kidunia itakavyokuwa jambo halisi hivi karibuni.

5 Ikiwa mwenye nyumba aonyesha shaka kuhusu kuwapo kwa Muumba, huenda ukasema:

◼ “Watu wengi wana maoni kama yako, hasa wanapoona kuteseka kote kunakoendelea ulimwenguni. Ikiwa kuna Mungu, kwa nini yeye angeruhusu kuteseka? Je! wewe unaweza kufikiria maelezo yoyote yanayofaa?” Ikitegemea itikio, unaweza kuendelea kwa kutumia sura ya 16 ya kitabu Creation ili kuendeleza mazungumzo. Majibu ya ziada yenye kusaidia ya swali hilo yaweza kupatikana katika kitabu Kutoa Sababu kurasa 137-8. Nyakati nyingine huenda ikafaa kuacha trakti Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia.

6 Kusudi letu si kuchochea tu kupendezwa na ujumbe wa Ufalme bali pia ni kuanzisha mafunzo ya Biblia. Jinsi tulivyo na furaha kuwa na kitabu hicho chenye vielezi vya kupendeza kinachoeleza ukweli kuhusu uumbaji na kumheshimu Muumba wetu Mtukufu! Na tukitumie vizuri katika kuchochea kupendezwa kwa watu wenye mioyo minyoofu tunaokutana nao wakati wa Septemba.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki