Sanduku la Swali
● Nani apaswa kushughulikia matangazo kwenye Mkutano wa Utumishi?
Lengo la sehemu hii ya Mkutano wa Utumishi ni kujulisha kundi mambo madogomadogo yenye maana kwa kutimiza huduma lililogawiwa. Baadhi ya matangazo hutumika kuwa vikumbusha nayo huwa ni yale yale juma baada ya juma. Hata hivyo, matangazo yote yapasa yasomwe waziwazi. Hapana yoyote yanayopasa kutendewa vivi hivi au kikawaida tu.
Hali ya baadhi ya matangazo huenda ikataka kwamba yatolewe na mzee. Inapokuwa hivyo, ni daraka la mwangalizi msimamizi apangie ndugu aliyestahili vizuri atoe habari hiyo, hata ingawa ndugu mwingine atashughulikia matangazo mengine yaliyoratibiwa.
Wakati barua yenye habari kwa kundi inapotia ndani habari nyingine inayoelekezwa kwa wazee peke yao, mzee mmoja apaswa atoe habari hiyo. Barua fulani-fulani kutoka kwa Sosaiti zenye mwelekezo hususa kwa kundi yafaa zaidi zisomwe na mzee aliyestahili. Barua kama hizo zaweza kuhusu kampeni za kuandika barua za pekee kwa niaba ya ndugu zetu wanaopatwa na mnyanyaso. Barua fulani-fulani zaweza kuwa na habari yenye mambo mengi madogomadogo juu ya utendaji wa kitheokrasi wa wakati ujao, kama vile ziara za mwangalizi wa mzunguko, makusanyiko, na mikusanyiko.
Huenda kukawa nyakati ambapo ni lazima kufanya matangazo ya maana kuhusiana na masilahi ya kundi, na ni lazima habari hiyo itolewe waziwazi. Yafaa zaidi matangazo kama hayo yafanywe na mzee.
Yawe yanatolewa na wazee au watumishi wa huduma, matangazo yapasa yatolewe kwa uwazi na kwa ufupi. Kufuata miongozo hii kutahakikisha kwamba maagizo kwa kundi yanaelezwa ifaavyo ili wote wasonge mbele kwa umoja.—Zab. 133:1; 1 Kor. 14:8, 9, 40.