Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/08 uku. 1
  • Ratiba Mpya ya Mkutano wa Kutaniko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Mpya ya Mkutano wa Kutaniko
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani Inayotimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Sanduku La Swali
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 10/08 uku. 1

Ratiba Mpya ya Mkutano wa Kutaniko

1, 2. Kutakuwa na mabadiliko gani kuhusiana na mikutano kuanzia Januari 2009?

1 Akina ndugu na dada ulimwenguni pote walisikia tangazo lenye kusisimua juma la Aprili 21-27, 2008. “Kuanzia Januari 1, 2009, Funzo la Kitabu la Kutaniko litafanywa pamoja na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi. Jina la Funzo la Kitabu la Kutaniko litabadilishwa na kuwa Funzo la Biblia la Kutaniko.”

2 Ratiba ya Mkutano Huo wa Kila Juma: Mkutano huo, kutia ndani nyimbo na sala, utafanywa kwa saa 1 na dakika 45. Mkutano utaanza kwa wimbo na sala (Dak. 5), na kufuatiwa na Funzo la Biblia la Kutaniko (Dak. 25). Mara tu baada ya funzo hilo, kutakuwa na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (Dak. 30). Kisha, kutakuwa na wimbo (Dak. 5) ambao utatanguliza Mkutano wa Utumishi (Dak. 35). Mkutano huo utamalizika kwa wimbo na sala (Dak. 5). Ili kuwasaidia kujitayarisha kwa ajili ya mikutano hiyo, ratiba ya Funzo la Biblia la Kutaniko, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, na ya Mkutano wa Utumishi itachapishwa kila mwezi katika Huduma Yetu ya Ufalme.

3. Funzo la Biblia la Kutaniko litaongozwa jinsi gani?

3 Funzo la Biblia la Kutaniko: Mkutano huo utaongozwa kama Funzo la Mnara wa Mlinzi. Hakutakuwa na haja ya kuanza kwa kurudia habari ya juma lililotangulia. Badala yake, utangulizi wa mkutano huo unapaswa kuwa mfupi sana. Kwa njia hiyo, kutakuwa na muda wa kutosha ili wote waliohudhuria watoe maelezo mafupi. Mwangalizi-msimamizi atakuwa na jukumu la kuwapa wazee migawo ya kuongoza mkutano huo, mzee tofauti kila juma.

4. Mkutano wa Utumishi utabadilika kwa njia gani?

4 Mkutano wa Utumishi: Mkutano wa Utumishi utaongozwa kama kawaida, lakini sehemu zake zitafupishwa. Kwa kawaida, Matangazo yatafanywa kwa dakika tano. Muda huo unatosha kwa ajili ya matangazo muhimu na barua fulani kutoka kwenye ofisi ya tawi. Matangazo kuhusu mipango ya utumishi wa shambani, mipango ya usafi, ripoti za hesabu, na barua kutoka kwenye ofisi ya tawi zinazohusu mambo ya kawaida hazitahitaji kusomwa jukwaani bali zitabandikwa kwenye ubao wa matangazo ili akina ndugu wajisomee. Wale waliogawiwa sehemu katika programu hiyo wanapaswa kujitayarisha vizuri na kufuata kabisa wakati na maagizo yaliyotolewa.

5. Wakati wa juma la ziara ya mwangalizi wa mzunguko, ratiba ya mikutano ya kutaniko itakuwaje?

5 Ziara ya Mwangalizi wa Mzunguko: Ratiba ya mwangalizi wa mzunguko ya kila juma haitabadilika. Jumanne, kutakuwa na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi ambao utafuatwa na wimbo. Kisha mwangalizi wa mzunguko atatoa hotuba ya dakika 30. Kama ilivyo sasa wakati wa juma la ziara yake, jioni nyingine itatengwa kwa ajili ya Funzo la Biblia la Kutaniko ambalo litafuatwa na wimbo na hotuba ya utumishi ya mwangalizi wa mzunguko. Mkutano huo utamalizika kwa wimbo na sala.

6. Mwangalizi wa kikundi ana majukumu gani?

6 Mikutano ya Utumishi wa Shambani: Baraza la wazee litawapa waangalizi wa vikundi mgawo wa kusimamia vikundi vya utumishi wa shambani na kuwafanyia ziara za uchungaji wale walio katika vikundi vyao. Mtumishi wa huduma akipewa mgawo wa kutekeleza majukumu hayo, basi ataitwa “mtumishi wa kikundi.”

7. Tunaweza kutazamia nini katika ratiba yetu mpya ya mikutano ya kutaniko?

7 Mipango hiyo inaonyesha kwamba tutakuwa na jioni ya karamu ya kiroho yenye kuelimisha na yenye kujenga. Hilo litatuwezesha kuwa wahubiri na walimu stadi, waliozoezwa ili kuzaa matunda zaidi katika huduma.—Efe. 4:13, 14; 2 Tim. 3:17.

8. Kujitayarisha kibinafsi mapema kutatunufaishaje sisi na wengine?

8 Kujitayarisha mapema kwa ajili ya mikutano hiyo kutatusaidia kukazia fikira mambo makuu yatakayokaziwa katika kila mkutano. Sote tutakuwa na nafasi ya kutoa maelezo, na hivyo kutiana moyo. (Rom. 1:11, 12; Ebr. 10:24) Tunapaswa kuwa na lengo la kufanya ‘maendeleo yetu yawe wazi’ kwa ‘kulitumia sawasawa neno la kweli.’—1 Tim. 4:15; 2 Tim. 2:15.

9. Tumeazimia kufanya nini, na kwa nini?

9 Tunafurahia sana mabadiliko hayo muhimu ya mikutano yetu ya kutaniko. Acheni sisi sote tuendelee kufuata mwongozo wa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” na kubaki karibu na Mchungaji wetu Mkuu anapotutayarisha kwa ajili ya ile “dhiki” kuu iliyo karibu sana.—Mt. 24:21, 45; Ebr. 13:20, 21; Ufu. 7:14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki