Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/90 uku. 4
  • Kutangaza Habari Njema Kwa Kutumia Ufahamu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutangaza Habari Njema Kwa Kutumia Ufahamu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUMWELEWA MWENYE NYUMBA
  • KUREKEBISHA MAHUBIRI
  • Kutoa Habari Njema—Kwa Utambuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Kushiriki kwa Mafanikio Katika Huduma Yetu ya Kuokoa Uhai
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Wasaidie Wengine Wajifunze Juu ya Mwana wa Mungu, Yesu Kristo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Onyesha Unawajali Watu Kikweli—Kwa Kubadilikana
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 3/90 uku. 4

Kutangaza Habari Njema Kwa Kutumia Ufahamu

1 Mtume Paulo alikazia uhitaji wa kutumia ufahamu katika kutangaza habari njema kwa watu wenye imani na malezi yenye kutofautiana. Katika siku yetu, watu wengine hudai kuwa wa kidini, na hali wengine hawana mbetuko wa kiroho wala hawathamini viwango vya kiroho. Tukiwa wahubiri wa habari njema, ni lazima tuufanye ujumbe wa Ufalme uvutie ‘watu wa aina zote’ kwa kutumia ufahamu katika huduma.—1 Kor. 9:19-23, NW.

KUMWELEWA MWENYE NYUMBA

2 Kutumia ufahamu katika utumishi wa shambani kunatia ndani uwezo wa kurekebisha mahubiri yetu kulingana na mapendezi ya mwenye nyumba. Hiyo inataka matayarisho mazuri. Kwa kuzoeleana kabisa na habari nyingi mbalimbali zinazozungumzwa katika vitabu na magazeti tuliyo nayo, mhubiri aweza kuwa tayari kutangaza habari njema akiwa na mambo mbalimbali ya kuongea juu yake. Tunapoongea na wenye umri mkubwa, vijana, vichwa vya jamaa, wake wa nyumbani, wanawake wanaofanya kazi ya kuajiriwa, na wengine, tunahitaji kufikiria mastakimu zao za kibinafsi na kutumia ufahamu katika kuchagua habari tutakayotoa.

3 Unapomfikia mwenye nyumba, uwe chonjo kuona mazingira. Huenda ukaweza kufahamu kwamba mwenye nyumba ni mzazi, wa malezi fulani ya kidini, anapendezwa sana na utunzaji wa nyumba yake, na kadhalika. Ukiwa na habari hiyo, unaweza kurekebisha utangulizi wako ufae mastakimu na mapendezi ya mwenye nyumba. Kwa maswali ya busara, ya akili na kusikiliza kwa makini maelezo ya mtu huyo, huenda ukaweza kufahamu imani na hisia zake halafu uamue njia ifaayo zaidi ya kuendelea na mahubiri yako.

KUREKEBISHA MAHUBIRI

4 Ikiwa ufikiapo nyumba unaona vitu vya kuchezea vya watoto au watoto, huenda ukaanza Kichwa cha Mazungumzo cha wakati huu kwa kusema: “Tumekuwa tukiongea na wazazi katika ujirani juu ya miongozo wanayoandalia watoto wao. Wazazi wengi wanahangaika juu ya ukosefu wa uongozi wa kiadili kwa ajili ya watoto katika ulimwengu wa leo. Je! wewe umekwisha kuona tatizo fulani katika jambo hilo?” Sikiliza itikio la mwenye nyumba. Ikiwa itikio linadokeza kwamba mwenye nyumba ana mwelekeo wa kidini, huenda ukaendelea hivi: “Ni jambo la kupendeza kwamba Biblia inataja juu ya uhitaji wa sisi na watoto wetu kupokea mwelekezo wa hekima. Angalia yanayosemwa hapa kwenye Mithali 14:12.” Baada ya kusoma andiko hilo, waweza kusema: “Nilikuwa nikisoma jambo fulani hivi karibuni lililokazia jinsi shauri la Biblia lilivyo lenye mafaa kwetu sisi.” Fungua ukurasa 174 wa The Bible—God’s Word or Man’s? na kusoma fungu la mwisho katika sura hiyo. Halafu toa kitabu hicho.

5 Ikiwa jibu la mwenye nyumba linadokeza kwamba yeye hathamini shauri la Biblia, unaweza kuonyesha ufahamu kwa kubadili mahubiri yako na kusema: “Nawez kukuuliza ni kwa nini ulifikia kukata maneno hivyo?” Baada ya kusikiliza jibu lake, huenda ukaendelea hivi: “Naweza kuelewa ni kwa nini unahisi hivyo. Kwa kweli, hivi karibuni nilisoma jambo fulani katika kichapo hiki ambalo n’na hakika litakupendeza.” Fungua ukurasa 6 na kusoma mafungu 3 na 4. Pia, soma sentensi ya kwanza katika fungu 5 kwenye ukurasa 7. Muulize mwenye nyumba kama angependa kuchunguza yale ambayo watu wengine hukubali kuwa uthibitisho wa kuwa Biblia ni halisi.

6 Tujitayarishapo vizuri na kuonyesha ufahamu katika utumishi wa Yehova, tutaweza kusema kama alivyosema mtume Paulo, “Mimi nimekuwa mambo yote kwa watu wa aina zote, ili niweze kwa njia zote kuwaokoa wengine.”—1 Kor. 9:22, NW; Mit. 19:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki