Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/05 uku. 1
  • Onyesha Unawajali Watu Kikweli—Kwa Kubadilikana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Onyesha Unawajali Watu Kikweli—Kwa Kubadilikana
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Kutangaza Habari Njema Kwa Kutumia Ufahamu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Onyesha Unawajali Watu Kikweli —Kwa Kujitayarisha
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Jinsi ya Kutumia Mapendekezo ya Kutoa Vichapo
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Jinsi ya Kutayarisha Utoaji wa Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2006
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 12/05 uku. 1

Onyesha Unawajali Watu Kikweli—Kwa Kubadilikana

1 Mtume Paulo aliweka mfano mzuri wa kubadili utoaji wake wa habari njema nyakati zote ili ufaane na malezi na kufikiri kwa wasikilizaji wake. (1 Kor. 9:19-23) Tunapaswa kujitahidi kufanya vivyo hivyo. Kwa kujitayarisha mapema, mara nyingi tunaweza kubadili mapendekezo yaliyo kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ili yafae hali za watu katika eneo letu. Tunapokaribia mlango, tunaweza kutambua mambo yanayompendeza mwenye nyumba kisha tunaweza kutumia mambo hayo katika utoaji wetu. Hata hivyo, kuna njia nyingine tunayoweza kubadilikana katika utumishi wetu.

2 Badilikana Kulingana na Yale Watakayosema: Mara nyingi tunapohubiri habari njema, sisi huwauliza wenye nyumba swali na kuwaalika wajibu. Sisi huitikiaje jibu lao? Je, ni kawaida yako kuitikia kijuujuu tu na kuendelea na utoaji uliotayarisha? Au je, kile unachosema huonyesha kwamba unafikiria jibu la wenye nyumba? Unapoonyesha upendezi wa kweli kwa yale ambayo wengine wanasema, huenda ukatumia maswali mengine yenye busara ili kujua kile ambacho hasa wanafikiria. (Met. 20:5) Hivyo, unaweza kuzungumzia ujumbe wa Ufalme unaoshughulikia hasa mahangaiko ya msikilizaji.

3 Ili kufanya hivyo tunapaswa kuwa tayari kuzungumzia mambo mengine mbali na yale tuliyokuwa tumepangia. Tukianza kwa kuzungumzia tatizo lililotajwa katika vyombo vya habari naye mwenye nyumba ataje tatizo katika ujirani au jambo la kibinafsi linalomhangaisha, tamaa yetu ya kutosheleza mahitaji yake itatuchochea tubadili mazungumzo yetu ya Biblia ili yapatane na habari inayompendeza zaidi.—Flp. 2:4.

4 Kubadili Mazungumzo Yetu: Mwenye nyumba anapouliza swali, huenda ikafaa kuendeleza mazungumzo hayo wakati mwingine baada ya kutafuta habari za ziada kuhusu jambo hilo. Tunaweza pia kumtolea vichapo vinavyozungumzia jambo hilo kwa undani. Yote hayo yanaonyesha tunapendezwa kikweli kuwasaidia wengine wamjue Yehova.—2 Kor. 2:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki