Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/05 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 12
  • Juma Linaloanza Desemba 19
  • Juma Linaloanza Desemba 26
  • Juma Linaloanza Januari 2
Huduma ya Ufalme—2005
km 12/05 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Desemba 12

Wimbo 32

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Novemba 15 na Amkeni! la Novemba 22 kwa kutumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 (yakifaa eneo lenu). Utangulizi mwingine unaofaa unaweza kutumiwa. Baada ya kila onyesho, taja jinsi ilivyo rahisi kutia ndani andiko katika mazungumzo.

Dak. 15: “Shule Ambayo Hutusaidia Kutumia Mambo Tunayojifunza.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Tia ndani maelezo kutoka nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2005.

Dak. 20: “Elimu Inayoongoza Kwenye Uzima.”a Panga mapema ndugu mmoja au wawili waeleze jinsi ambavyo wamenufaika kwa kujifunza kumhusu Mungu kupitia tengenezo lake.

Wimbo 101 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 19

Wimbo 160

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Taja mipango ya pekee ya utumishi wa shambani kwa ajili ya Desemba 25 na Januari 1. Wakumbushe wote waje na gazeti la Amkeni! la Januari 2006 kwenye Mkutano wa Utumishi juma lijalo.

Dak. 15: “Onyesha Unawajali Watu Kikweli—Kwa Kubadilikana.”b Tia ndani onyesho fupi kuonyesha jinsi mhubiri anavyoweza kubadili mazungumzo yake ikitegemea maelezo ya mwenye nyumba.

Dak. 25: “Je, Mtoto Wako Anaweza Kufanya Uamuzi Mzito?”c Ishughulikiwe na mzee. Panga mafungu yote yasomwe kwa sauti na ndugu aliye msomaji mzuri. Zungumzia maandiko yote yaliyotajwa. Baada ya kuzungumzia fungu la 2, onyesha tofauti iliyopo kati ya vijana wawili waliotajwa katika fungu la 16 na 17 na kwenye sanduku katika ukurasa wa 16 na 17 wa gazeti Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 1991. Kwa kumalizia, watie moyo wazazi warudie makala yote katika gazeti hilo pamoja na watoto wao na mara moja wazungumzie na kufanya mazoezi pamoja na watoto wao kuhusu amri ya Biblia kuhusu damu ili watoto waweze kueleza imani yao kwa usadikisho. Vichwa vya familia wanapaswa kuhakikisha kwamba kila mtoto aliyebatizwa anabeba kadi yake ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia na kila mtoto asiyebatizwa anabeba Kadi ya Utambulisho. Mtu anapolazwa hospitalini na suala la kutiwa damu mshipani lizuke, wazee wanapaswa kuwasiliana na Halmashauri ya Uhusiano na Hospitali.

Wimbo 56 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 26

Wimbo 85

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za Desemba. Ikiwa kutaniko lenu litabadili saa za mikutano mwaka ujao, taja badiliko hilo. Taja toleo la Januari, na kuonyesha mahali ambapo madokezo ya kutoa toleo hilo yanaweza kupatikana.

Dak.15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: Sura Mpya ya Amkeni! Hotuba pamoja na mazungumzo na wasikilizaji. Taja mabadiliko katika Amkeni! kama ilivyotangazwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 2005, ukurasa wa 1, fungu la 5-6. Tia ndani maelezo kutoka makala “Kwa Wasomaji Wetu” katika gazeti la Amkeni! la Januari 2006, ukurasa wa 3-4. Onyesha mifano ya jinsi ambavyo gazeti hilo linawaelekeza wasomaji moja kwa moja kwenye Biblia. Waalike wasikilizaji watoe maoni yao kuhusu makala mpya kwenye ukurasa wa 31. Tutaendelea kuwatolea watu magazeti yote mawili, Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yakiwa pamoja katika ziara ya kwanza. Bila shaka, tutawaachia watu tunaowapelekea magazeti yetu kwa ukawaida nakala moja tu ya kila toleo la Amkeni! Panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na Amkeni! la Januari ikiwa yanapatikana. Utangulizi mwingine unaofaa unaweza kutumiwa. Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari itatoa mapendekezo mengine ya jinsi ya kutoa gazeti Amkeni! la Januari ikikazia makala nyingine katika gazeti hilo. Mapendekezo yote mawili yanaweza kutumiwa mwezi wote.

Wimbo 222 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 2

Wimbo 5

Dak. 7: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 18: “Tumia kwa Hekima Vichapo Vyetu Vinavyotegemea Biblia.”d Tia ndani maelezo kutoka kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2002, ukurasa wa 1.

Dak. 20: “Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova la 2006 la ‘Ukombozi Unakaribia.’”e Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Watie moyo wote wafanye mipango mapema iwezekanavyo ili wahudhurie kusanyiko.

Wimbo 48 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki