Habari za Kitheokrasi
◆ Wakati wa miezi ya Oktoba na Novemba, mikusanyiko ya wilaya 28 ilifanywa katika Arjentina ikiwa na hudhurio la 130,262. Wahubiri 79,858 walioripoti utendaji Novemba wanawakilisha kilele kipya kisichopata kufikiwa tena.
◆ Aisilandi iliripoti kilele kipya cha wahubiri 233 katika Novemba. Kulikuwako hudhurio la 382 kwenye siku ya pekee ya kusanyiko la hivi karibuni.
◆ Ailandi iliripoti kilele cha 20 cha mfululizo cha wahubiri 3,255 wakati wa Novemba. Ilitia moyo kuona kwamba 78 walibatizwa kwenye mfululizo wa hivi karibuni wa siku za pekee za kusanyiko.
◆ Madagaska ilikuwa na ongezeko la asilimia 8 katika Novemba na kilele kipya cha wahubiri 3,424 wakiripoti.
◆ St. Maarten ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 141 katika Novemba, ongezeko la asilimia 17. Siku yao ya pekee ya kusanyiko ilihudhuriwa na 282.
◆ Zimbabwe ilifikia kilele kipya cha wahubiri 17,113 Novemba. Wanaongoza jumla ya mafunzo ya Biblia 19,190.
◆ Darasa la tano la Shule ya Mazoezi ya Kihuduma katika United States lilihitimu katika Los Angeles, Kalifornia siku ya Jumapili, Januari 14, 1990. Wahitimu 20 walipewa mgawo wa kutumikia katika mabara sita tofauti-tofauti nje ya United States.