Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/90 kur. 1-4
  • Toa Ushahidi kwa Ukweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Toa Ushahidi kwa Ukweli
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MGAWO WETU WA MUHIMU
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Mradi Mzuri kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Je, Tutaufanya Tena?—Mwito Mwingine wa Mapainia-Wasaidizi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Je! Wewe Unaweza Kufanya Upainia Msaidizi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 5/90 kur. 1-4

Toa Ushahidi kwa Ukweli

1 Yesu alibainisha kwamba alikuwa amekuja katika ulimwengu ili kutoa ushahidi kwa ukweli. Yeye alitangaza rasmi hivi: “Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili nishuhudie kweli.”—Yohana 18:37.

2 Kwa kuhubiri kwake kwa bidii, Yesu aliheshimu jina la Yehova. Yeye pia alionyesha upendo halisi kwa ajili ya watu kwa kutambua hali yao ya kiroho yenye kusikitisha. Mathayo aliandika kuhusu utendaji wake: “Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme . . . Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanywa kama kondoo wasio na mchungaji.” (Mt. 9:35, 36) Kama vile Yesu, ujitoaji wetu kwa Yehova pamoja na upendo wetu kwa ajili ya wengine vyapasa kutusukuma tuhubiri.

MGAWO WETU WA MUHIMU

3 Upendo halisi kwa ajili ya watu na kwa ajili ya Yehova hutuchochea sisi tutumie kwa faida kila fursa ili kufundisha watu ukweli juu ya Yehova na kazi zake za ajabu. (Zab. 96:2, 3; 145:10-13) Hata hivyo, mikazo ya maisha ya kila siku, mahangaiko ya maisha, na utele wa vikengeusho vyaweza kutuondosha kwenye utendaji wetu wa kutoa ushahidi. Kwa hiyo, tunahitaji kukazia uharaka wa kutoa ushahidi kwa ukweli juu ya Mungu na Ufalme wake. Hatupaswi kujiruhusu tukengeushwe kutoka kwa kazi hii ya maana zaidi ya kuokoa uhai ambayo tumegawiwa. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Kujishughulisha katika utumishi wa Yehova ni himaya kwa ajili yetu, na kwaweza kuleta manufaa za kudumu kwa wale wanaohitaji kusikia ujumbe wa ukweli.—1 Kor. 15:58.

4 Je! wewe waweza kutumika ukiwa painia wa kawaida au msaidizi? Kwa nini usichunguze mambo yako uone kama waweza kupanua utumishi wako katika njia hiyo? Je! umestaafu kazi ya kimwili? Kwa nini usitumie wakati wako kwa ukamili zaidi katika kuhubiri? Wachanga wengi ambao wangali shuleni wamefanya upainia msaidizi kwa ukawaida. Wao wameona hilo laburudisha kiroho na kimwili pia, likileta shangwe ya moyo.

5 Kutoa ushahidi kwa ukweli kwa njia yenye matokeo kwataka kuratibu kwa uangalifu wakati wetu. (Efe. 5:15, 16) Kufanya upainia msaidizi kwataka wastani wa saa mbili tu kwa siku kila mwezi. Wengine huchagua kuamka saa moja mapema ili watoke nje katika utumishi kabla ya kwenda shuleni au kazini. Makundi mengi yamesaidia mapainia wasaidizi kwa kupanga utoaji ushahidi wa alasiri au jioni. Pia, waweza kutiwa moyo na kupata madokezo yenye kusaidia kwa kuongea na wengine ambao wamefanya vema katika kuratibu wakati wao ili wafanye upainia msaidizi.

6 Yehova Mungu ameonyesha wema watumishi wake sikuzote. Wale wanaomtumikia katika uaminifu wamepokea baraka kwa utele sana. Wema wa Yehova ungali unaonyeshwa kuelekea wale wanaompenda. Yeye apendezwa kupokea chochote ambacho mambo yetu yaturuhusu kufanya tutoapo ushahidi kwa ukweli.—Ebr. 6:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki