Habari za Kitheokrasi
◆ Mnamo Januari 23, 1990, serikali ya Benin ilitangua kirasmi marufuku juu ya kazi ya Mashahidi wa Yehova katika nchi hiyo. Mnamo Januari 28 akina ndugu waliona shangwe kuweza kukutana pamoja kwa ajili ya mkutano wa pekee uliofanywa katika Cotonou, na sasa wanatazamia kuzidisha kazi yao ya kitheokrasi.
◆ Kolombia yaendelea kuripoti ukuzi mzuri. Wakati wa Januari walifikia kilele kipya cha wahubiri 43,850, na 490 wakabatizwa.
◆ Mnamo Januari 26, 1990, kibali kilitolewa kwa ajili ya ujenzi wa Jumba la Kusanyiko la kwanza katika Costa Rica. Litakuwa na viti 2,200 na latazamiwa kukamilishwa katika muda wa mwaka mmoja.
◆ Mnamo Machi 14, 1990, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Ujeremani (Ujeremani ya Mashariki) ilitoa hati yenye kutoa uhuru wa kidini kwa Mashahidi wa Yehova katika bara hilo na kuhalalisha kazi yao. Shukrani ni kwa Yehova, kuwa ndugu zetu huko wanashiriki kwa furaha na kwa bidii katika huduma kwa uwazi.