Habari za Kitheokrasi
◆ Chile iliripoti kilele kipya ambacho hakijapata kufikiwa cha wahubiri 36,968 katika Juni. Hilo lilikuwa ongezeko la asilimia 12 kupita wastani wa mwaka jana. Kilele kipya cha mafunzo ya Biblia nyumbani 53,967 kiliripotiwa pia.
◆ Ripoti ya wahubiri katika Juni ya Jamhuri ya Muungano ya Ujeremani inaonyesha ongezeko la asilimia 4 kupita wastani wa mwaka jana. Jumla la 131,106 waliripoti.
◆ India iliripoti kilele kipya cha wahubiri 10,272 kwa mwezi Juni. Hilo ni ongezeko la asilimia 17 kupita wastani wa mwaka jana. Pia kulikuwako kilele kipya katika mapainia wa kawaida, ziara za kurudia, na mafunzo ya Biblia.
◆ Réunioni ilikuwa na ongezeko la asilimia 18, ikiwa na wahubiri 1,833 wakiripoti katika Juni. Walikuwa na vilele vipya katika ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia pia.