Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/91 uku. 3
  • Kumsifu Yehova kwa Wimbo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kumsifu Yehova kwa Wimbo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Mwimbie Yehova Sifa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Thamani ya Kuimba Katika Ibada ya Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Imba kwa Shangwe na Sauti Kubwa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Mahali pa Muziki Katika Ibada ya Kisasa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 2/91 uku. 3

Kumsifu Yehova kwa Wimbo

1 Tafadhali fungua kitabu chako cha nyimbo kwenye karatasi ya mwisho. Waona nini? Korasi ya waimbaji Walawi kwenye hekalu takatifu la Yehova, vinywa vyao vikiwa vimefumbuliwa wazi, wakiimba kwa idili. Kuimba kulikuwa sehemu yenye maana katika ibada ya kweli kwenye hekalu la Yehova. Wakati wa Mfalme Daudi, zaidi ya asilimia 10 ya wale waliotumikia hekaluni walipewa mgawo wa kumsifu Yehova kwa muziki. Na kati ya hesabu hiyo, 288 walikuwa waimbaji waliozoezwa, ‘wote wakiwa stadi.’ Waweza kuwa na hakika wao walikuona kuimba kwao kwa uzito.—1 Nya. 23:3, 5; 25:7.

2 Tukija katika nyakati za Kikristo, twajifunza kwamba Yesu na mitume wake waliimba wimbo mwishoni mwa Chakula cha Bwana cha Jioni. (Mk. 14:26) Na mtume Paulo hutuambia kwa kurudia-rudia tumwimbie Mungu wetu sifa. Kwenye Wakolosai 3:16 aliandika hivi: “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.”—Ona pia Waefeso 5:19, 20.

3 Kuimba nyimbo za Ufalme ni njia moja ambayo katika hiyo sisi twamsifu Yehova. Hivyo basi, je, haitupasi kuimba kwa mioyo yetu yote? Tufanyapo hivyo, twampa Yehova sifa. Yeye husikiliza nyimbo zetu zinazoelekezwa kwake kama vile anavyofanya kwa sala zetu. Tuimbapo kwa moyo kweli kweli, twaweza pia kuletea wengine shangwe, na sisi wenyewe twanufaika.

4 Fikiria maneno mazuri ya nyimbo zetu. Kwa kweli hayo ni msaada katika ‘kufundishana na kuonyana.’ Nyimbo zetu zina shauri bora kama nini! Kwa kuchukua shauri hilo kwa uzito, twaweza kusaidiwa tusitawishe tunda la roho, ili tuwe nalo kwa wingi na kujilinda tusiingiliwe na mavutano ya kimwili, ya kilimwengu. ‘Kuimba katika mioyo yetu’ hututia moyo tumtumikie Yehova kwa ujasiri na kwa uchangamfu.

5 Ili kuanzisha wimbo vizuri kwenye mikutano, mwenyekiti aweza kutangaza si namba tu bali pia na kichwa, au jina la wimbo, Pindi kwa pindi aweza kuangalia pia msingi wa Kimaandiko wa wimbo na kutoa maelezo kifupi jinsi unavyopatana na habari inayotolewa.

6 Kingdom Melodies na pia kaseti za piano za nyimbo zetu ni vyombo vizuri sana vya kusaidia familia zetu zifahamu vizuri nyimbo. Kuzitumia kuwa muziki wa sauti ya chini tunapofanya mambo mengine ni njia yenye kuleta sana shangwe ya kutufanya tuzihamu zaidi nyimbo zetu.

7 Maandiko hutukumbusha kwa kurudia-rudia juu ya wajibu wetu wa kumsifu Baba yetu wa kimbingu mwenye upendo. Na tufanye hivyo kwa nafsi yote. Hivyo twaweza kutolea ushuhuda wenye kuwachangamsha moyo wageni ambao huja kati yetu. Ndiyo, acheni sisi tuimbe na kumsifu Yehova kwa melodia kama alivyofanya Daudi wa nyakati za kale.—Zab. 108:1-3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki