Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/91 uku. 2
  • Mikutano Inayotusiadia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusiadia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA JULAI 1
  • JUMA LINALOANZA JULAI 8
  • JUMA LINALOANZA JULAI 15
  • JUMA LINALOANZA JULAI 22
  • JUMA LINALOANZA JULAI 29
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 7/91 uku. 2

Mikutano Inayotusiadia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA JULAI 1

Wimbo 173

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Kazia makala katika magazeti ya karibuni zinazoweza kutumiwa katika kazi ya magazeti Jumamosi hii.

Dak. 15: “Tumia Kikamili Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Changanueni kirefu mambo katika fungu la 3 na la 4 kadiri wakati uruhusuvyo.

Dak. 20: “Uwe Mwenye Subira na Kufanya Huduma Kikamili.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Baada ya kuzungumza fungu la 6, mhubiri atoe wonyesho wa jinsi ya kutumia Kichwa cha Mazungumzo wakati wa kutoa broshua “Tazama!”

Wimbo 156 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JULAI 8

Wimbo 162

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Habari za Kitheokrasi. Likumbushe kundi mipango ya utumishi wa shambani ya mwisho wa juma.

Dak. 15: “Uwe Mwenye Nafsi Yote Katika Huduma ya Shambani—Sehemu ya 1.” Mazungumzo ya maswali na majibu yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Toa mgawo kimbele maandiko makuu yaliyoteuliwa yasomwe, na kufanya matumizi yafaayo kwa kundi lenu. Amsha kupendezwa katika mfululizo huu wenye sehemu tano.

Dak. 20: Utumishi wa Wakati Wote—Fursa Nzuri Sana ya Kutembea Pamoja na Mungu. (Mika 6:8) Mzee anayestahili, au mtumishi wa huduma, ni afadhali zaidi akiwa katika utumishi wa wakati wote, atoa hotuba yenye uchangamfu, na yenye kutia moyo. (Ona Mnara wa Mlinzi wa Mei 15, 1989, kurasa 21-3.) Toa madokezo yenye kutumika ili kusaidia wahubiri wa kundi, kulingana na hali zao, wafikirie kwa uzito kuingia katika kazi ya wakati wote. Hoji mapainia wawili au watatu, na kuonyesha zile manufaa nyingi za utumishi wa wakati wote. Mwaka mpya wa utumishi ni wakati unaofaa kuanza. Wale wanaoanza kufikia Septemba 1, 1991, waweza kustahili kwenda kwenye Shule ya Utumishi wa Painia karibu na mwisho wa mwaka mpya wa utumishi.

Wimbo 204 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JULAI 15

Wimbo 32

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ikiwa makundi yatapokezana zamu za nyakati za mikutano katika Septemba 1, tangaza ratiba itakayofuatwa. Pitia mambo makuu ya ripoti ya kundi ya utumishi wa shambani ya Juni. Wapongeze wahubiri kwa yaliyotimizwa shambani.

Dak. 20: “Kutoa Habari Njema—Kwa Utambuzi.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Toa wonyesho wa mambo makuu katika fungu la 5. Mhubiri stadi aonyeshe jinsi ya kushughulika na mwenye nyumba ambaye mwanzoni ni mwenye ubishi kwa kumwuliza maswali kwa busara na kuonyesha yale ambayo Biblia husema juu ya habari hiyo. Wonyesho huo wapasa uwe umefanyiwa mazoezi vizuri.

Dak. 15: Jinsi Nilivyopata Kweli. Mambo yaliyoonwa. Mzee ahoji watu wawili au watatu. Kazia jinsi Neno na tengenezo la Mungu lilivyowahimiza kufikia wakfu na ubatizo. Kazia manufaa wanazopata kwa kuwa katika kweli.

Wimbo 67 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JULAI 22

Wimbo 210

Dak. 15: Mzee au mtumishi wa huduma anayestahili ashughulikie matangazo ya kwenu. Waombe wasikilizaji mambo ya kuzungumzia kutokana na broshua zinazopatikana. Chagua mambo yanayopatana na Kichwa cha Mazungumzo na ambayo yatajenga katika mwenye nyumba taraja la kusoma broshua. Kuwe na wonyesho mfupi wa kuingia kutoka Kichwa cha Mazungumzo hadi kwenye broshua na jambo lifaalo la kuzungumzia.

Dak. 18: “Mpango wa Funzo la Kitabu la Kundi—Sehemu ya 1.” Mazungumzo yakiongozwa na mzee mwenye ujuzi pamoja na mzee mwingine mmoja au wawili au watumishi wa huduma ambao ni viongozi wa Funzo la Kitabu la Kundi. Tia mkazo wa pekee kwenye mambo mawili au matatu ambayo yanahitajiwa hasa katika kundi lenu, kama vile mtu kutoa maelezo kwa maneno yake mwenyewe na kufanya matumizi yenye mafaa ya habari inayozungumzwa.

Dak. 12: Mahitaji ya kwenu. Zungumza mambo ambayo wazee wahisi kwamba kundi lahitaji usaidizi. Waweza kufikiria Kimaandiko baadhi ya mambo ambayo fikira za kundi zilielekezwa kwayo wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko.

Wimbo 42 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JULAI 29

Wimbo 56

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Omba mambo yaliyoonwa kuhusu kuangusha broshua na kuanzisha mafunzo ya Biblia.

Dak. 15: Kupanga Kimbele kwa Ajili ya Mambo Mazuri ya Kiroho. Mwangalizi msimamizi azungumze pamoja na wasikilizaji mipango inayohitaji kufanywa kwa ajili ya miezi inayokuja, kutia na ushiriki kamili katika kampeni ya maeneo yaliyo peke yake, kuhudhuria programu ya Siku ya Kusanyiko la Pekee, (mipango ya kusafiri ikihitajiwa, kujitayarishia ubatizo kwa wale wanaotazamiwa kubatizwa, na kadhalika), na kufanya upainia msaidizi katika Agosti.

Dak. 15: “Tanguliza Mungu Katika Maisha ya Familia Yako!” Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Mei 15, 1991, kurasa 4-7.”

Wimbo 132 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki