Wimbo 210
‘Hakikisheni Mambo Yaliyo ya Maana Zaidi’
1. Tunatumikia Yehova;
Ndiye twapenda.
Upendo ni wa maana;
Watoka kwa Mungu.
Na uzidi tunapohakikisha mambo
Ya adili na ya kweli.
Nasi tuwe bila kosa,
tufanye kazi ya Mungu.
2. Mungu anataka tuwe
Watu wa shukrani,
Tutii yeye na
kushika ukamilifu.
Tuishi kwa amani na wote tuwape
Tumaini la Ufalme
—Tutende mema, tusiwakwaze,
tuwasaidie.
3. Muhimu ni kupamba
mafundisho ya Mungu,
Twende kama wadogo,
tufuate shauri.
Na tuwe waadilifu,
tuchangamuke Katika kazi ya Mungu.
Hivyo twahakikisha
mambo ya maana zaidi.