Kufanya Kazi Ngumu ili Kutenda Mapenzi ya Mungu
1 Kazi ngumu yenye kusudi inayopata matokeo yanayotakiwa ni yenye kuridhisha sana. (Mhu. 3:13) Ni kazi gani inayofanywa leo inayoweza kuleta furaha nyingi sana sasa na kuendelea hadi wakati ujao usiodhahiri? Kuna jibu moja tu—kufanya mapenzi ya Mungu. Sababu za hilo zitachunguzwa kikamili kwa njia ya hotuba, maonyesho, na mambo yaliyoonwa katika programu yetu ya siku ya kusanyiko la pekee kwa mwaka wa utumishi wa 1992. Kichwa cha programu kitakuwa “Kufanya Kazi Ngumu ili Kutenda Mapenzi ya Mungu.”—Efe. 6:6; 1 Tim. 4:10.
2 Wengi leo hawajaridhika kwa vyovyote na wanafadhaishwa na yale wametimiza maishani, sehemu kubwa ikiwa ni kazi wasiyofurahia. Kwa kutofautisha, kufanya mapenzi ya Yehova kwa kumwiga Kristo hufanya maisha zetu ziwe na kusudi na kunatuwezesha hata kufanya kazi zetu za kimwili tukiwa na mtazamo chanya. Ni nini kinachotiwa ndani katika kujitahidi kufanya mapenzi ya Mungu? Ni lazima tujilinde dhidi ya mambo gani ili tuendelee kuishi kwa ajili ya mapenzi ya Mungu? Kuhusiana na utendaji wetu wa kuhubiri na kufundisha, ni jambo la maana kadiri gani kufuata miongozo na madokezo yanayotolewa na tengenezo la Yehova? Vijana wanaokazia fikira kufanya mapenzi ya Mungu wana fursa gani za pekee?
3 Maswali hayo yatajibiwa vya kutosha na programu hiyo, inayotia ndani hotuba mbili za msingi “Je! Mapenzi ya Mungu Huongoza Maisha Yako?” na “Kusudi Letu Maishani—Kufanya Mapenzi ya Mungu.” Panga sasa uwepo na ufurahie kikamili programu hiyo ya pekee.