Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/11 uku. 3
  • ‘Mapenzi ya Mungu na Yatendeke’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Mapenzi ya Mungu na Yatendeke’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Linda Dhamiri Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • ‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Neno la Mungu Ni Lenye Faida kwa Kufundisha
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Sikiliza na Ujifunze
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 8/11 uku. 3

‘Mapenzi ya Mungu na Yatendeke’

1. Kichwa cha programu ya kusanyiko la pekee la mwaka wa utumishi wa 2012 ni gani, na kwa nini inafaa tufikirie habari hiyo?

1 Tuliumbwa kwa sababu ya mapenzi ya Yehova. (Ufu. 4:11) Hivyo, bila kujifunza na kufanya mapenzi ya Mungu, hatuwezi kuishi maisha yenye kusudi. Jambo hili si rahisi kwa sababu tunapaswa kupambana na mwelekeo wa ndani tulio nao wa kufanya “mambo yanayopendwa na mwili na fikira” au “mapenzi ya mataifa.” (Efe. 2:3; 1 Pet. 4:3; 2 Pet. 2:10) Bila msaada wa Mungu, tutakuwa hata tukijiweka katika hatari ya ‘kushikwa tukiwa hai na Ibilisi kwa ajili ya mapenzi ya huyo.’ (2 Tim. 2:26) Programu yetu ya kusanyiko la pekee la mwaka wa utumishi wa 2012 itasaidia kila mmoja wetu kutenda kulingana na ombi la tatu kuu katika ile sala ya kielelezo, yaani, “mapenzi yako na yatendeke.”—Mt. 6:9, 10.

2. Ni maswali gani yatakayojibiwa wakati wa programu hiyo?

2 Maswali Yatakayojibiwa: Utakapokuwa ukisikiliza programu, tafuta majibu ya maswali haya: Mbali na kusikiliza Neno la Mungu, ni jambo gani lingine muhimu tunalopaswa kufanya? Ni jinsi gani tunavyoweza kuendelea kutambua yale yaliyo mapenzi ya Mungu kwetu? Kwa nini tunapaswa kuwa tayari kuwasaidia watu wa namna zote? Tunaweza kupataje maisha yenye kuridhisha? Vijana, mnahitaji kumthibitishia Yehova nini? Tunapata thawabu gani kwa kufanya mapenzi ya Mungu? Kwa nini ni muhimu sana kwamba tuwajenge na kuwatia moyo wengine?

3. Tunaweza kufaidika jinsi gani na uandalizi huo wa kiroho?

3 Hakikisha unahudhuria na kusikiliza programu kwa makini. Yaelekea, msemaji anayezuru ni mwakilishi wa Betheli au mwangalizi anayesafiri. Kabla na baada ya programu, jihisi huru kuzungumza naye au mke wake, ikiwa ameoa. Mnaporudi nyumbani, msiwe ‘wasikiaji wasahaulifu,’ bali pitieni programu mkiwa familia na mzungumzie jinsi mnavyoweza kujitahidi hata zaidi kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu.—Yak. 1:25.

4. Kwa nini ni muhimu tutangulize mapenzi ya Mungu maishani?

4 Hivi karibuni, wale wanaofuatia tamaa zao na wanaokataa kufanya mapenzi ya Yehova, wataharibiwa. (1 Yoh. 2:17) Kwa hiyo, tunashukuru kwamba Yehova ametutayarishia habari hii ya wakati unaofaa ili kutusaidia kutanguliza mapenzi ya Mungu maishani!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki