Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/10 uku. 2
  • ‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Programu ya Kusanyiko la Pekee la Mwaka wa 2010
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Neno la Mungu Lina Nguvu
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Mpango Mpya wa Kupitia Programu za Makusanyiko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee
    Huduma ya Ufalme—2006
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 8/10 uku. 2

‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’

1. Programu ya hivi majuzi ya kusanyiko la pekee ilikusaidiaje wewe na wengine?

1 Mara nyingi baada ya kuhudhuria kusanyiko la pekee, tunasema, “Kwa kweli tulihitaji programu hiyo!” Mwangalizi mmoja wa mzunguko alisema kwamba baada ya kusikiliza programu ya hivi majuzi, baadhi ya wahubiri katika mzunguko wake walisema kwamba wangependa kutumia wakati mwingi zaidi katika huduma. Mwangalizi fulani asafiriye alisema, “Programu hiyo ilitusaidia kufikiri kwa njia inayofaa kuhusu nyakati tunamoishi tunapofanya maamuzi maishani.” Mwingine akasema, “Wahubiri wengi walieleza kwamba programu hiyo iliwasaidia kutambua umuhimu wa kuzingatia mambo yaliyo ya maana zaidi, yaani, huduma.” Kusanyiko la pekee lilikusaidiaje?

2. Ni habari gani zitakazozungumziwa katika programu ya mwaka ujao wa utumishi?

2 Mwaka ujao wa utumishi, tutakuwa na programu ambayo pia tunaihitaji kikweli. Kichwa cha programu hiyo ni ‘Pata Kimbilio kwa Yehova,’ kinachotegemea Zaburi 118:8, 9. Hizi ni baadhi ya habari zitakazozungumziwa: “Jinsi Yehova Anavyokuwa Ngome Wakati wa Taabu,” “Wasaidie Wengine Wapate Kimbilio Chini ya Mabawa ya Yehova,” “Mwige Yehova kwa Kuwaandalia Wengine Kimbilio,” “Enyi Vijana, Mfanyeni Yehova Kuwa Tegemeo Lenu!” na “Paradiso Yetu ya Kiroho—Kimbilio Ambalo Yehova Ameandaa.”

3. Tunaweza kunufaikaje kikamili kwa kuhudhuria kusanyiko lijalo?

3 Jinsi ya Kunufaika na Programu: Mara tu baada ya tarehe ya kusanyiko kutangazwa, fanya mipango hususa ya kuhudhuria na uwaalike wanafunzi wako wa Biblia wajiunge nawe. Ili ‘tuzae matunda kwa uvumilivu,’ tunapaswa kuyahifadhi mambo tunayosikia. (Luka 8:15) Hivyo basi, sikiliza programu kwa makini na uandike kifupi mambo makuu na mambo ambayo umepanga kutumia katika maisha yako na huduma yako. Tenga wakati baada ya kusanyiko mzungumzie programu hiyo mkiwa familia, na ufikirie njia hususa ambazo wewe na familia yako mwaweza kutumia habari hiyo.

4. Kwa nini tutazamie kwa hamu kusanyiko la pekee lijalo?

4 Kama chakula kitamu na chenye lishe, kusanyiko la pekee la mwaka huu limetayarishwa kwa upendo na ufikirio mwingi. Yehova na abariki jitihada zako za kuhudhuria na kunufaika na ‘chakula kwa wakati unaofaa’ cha kuwalisha kiroho wahudumu Wakristo.—Mt. 24:45.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki