Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/13 uku. 2
  • Neno la Mungu Lina Nguvu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Neno la Mungu Lina Nguvu
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Programu ya Kusanyiko la Pekee la Mwaka wa 2010
    Huduma ya Ufalme—2009
  • ‘Chakula kwa Wakati Unaofaa’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 8/13 uku. 2

Neno la Mungu Lina Nguvu

1. Programu ya kusanyiko la pekee la mwaka wa utumishi wa 2014 ina kichwa gani?

1 Tofauti na kitu kingine chochote kutoka kwa wanadamu ambao si wakamilifu, Biblia ina nguvu ya kutubadili na kufanya mawazo na njia zetu zipatane na mapenzi ya Yehova. Neno la Mungu lina nguvu kadiri gani? Tunaweza kutumiaje nguvu za Neno la Mungu maishani mwetu? Tunaweza kulitumiaje kwa njia nzuri kuwasaidia wengine? Tuna hakika kwamba sote tutafaidika mambo hayo yatakapozungumziwa kwenye kusanyiko la pekee la mwaka wa utumishi wa 2014. Kichwa cha kusanyiko hilo ni “Neno la Mungu Lina Nguvu,” kinachotegemea andiko la Waebrania 4:12.

2. Tunapaswa kutafuta majibu ya maswali gani?

2 Tafuta Majibu ya Maswali Yafuatayo: Utakapokuwa ukisikiliza programu tafuta majibu ya maswali yafuatayo.

• Kwa nini tunapaswa kutumaini Neno la Yehova? (Zab. 29:4)

• Tunawezaje kujionea nguvu za Neno la Mungu maishani mwetu? (Zab. 34:8)

• Unawezaje kuruhusu nguvu za Neno la Mungu ziwasaidie wale unaowahubiria? (2 Tim. 3:16, 17)

• Tunawezaje kuepuka kudanganywa na ulimwengu wa Shetani? (1 Yoh. 5:19)

• Vijana, mnawezaje kufanikiwa kuwa na uhusiano mzuri na Mungu? (Yer. 17:7)

• Tunawezaje kuwa na nguvu hata tunapokuwa dhaifu? (2 Kor. 12:10)

• Ni nini kitakachotusaidia tuendelee kufanya mabadiliko licha ya kwamba tulikuwa na mitazamo isiyofaa au tulikuwa na mazoea ya kufanya mambo mabaya? (Efe. 4:23)

3. Pamoja na kusikiliza programu, ni katika njia gani nyingine tunaweza kufaidika kutokana na kusanyiko la pekee?

3 Tutafaidika sana tutakaposikiliza programu hiyo! Pia, kama vile tu kusanyiko la mzunguko na la wilaya, katika kusanyiko la pekee tutapata fursa ya kufurahia ushirika wa ndugu na dada zetu kutoka makutaniko mengine. (Zab. 133:1-3; 2 Kor. 6:11-13) Kwa hiyo tenga wakati wa kushirikiana na marafiki wako wa muda mrefu, na utafute marafiki wengine. Ikiwa kuna msemaji anayezuru kama vile mwangalizi wa wilaya au ndugu kutoka Betheli ambaye amepewa mgawo kwenye kusanyiko la pekee unalohudhuria, kwa nini usimkaribishe yeye na mke wake? Kwa kweli, tuna sababu nyingi za kutazamia kwa hamu kusanyiko hilo la pekee!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki