Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
Uandalizi wa programu za siku ya pekee ulianza mwaka wa 1987. Mikusanyiko hii ya siku moja imethibitika kuwa yenye kujenga kwa watumishi wa Yehova na kwa watu wenye kupendezwa wanaohudhuria. Kuanzia Septemba 1998, programu mpya ya siku ya kusanyiko la pekee itatolewa. Utaona hotuba tisa na mahoji kadhaa na mambo yaliyoonwa kuwa yenye mafaa kiroho.
“Thamini Meza ya Yehova” ndicho kichwa cha programu hiyo mpya. (Isa. 65:14; 1 Kor. 10:21) Itaimarisha azimio letu la kwamba kumwabudu Yehova lazima kutangulizwe katika maisha yetu. (Zab. 27:4) Sehemu ya mwangalizi wa mzunguko itashughulika na “Kuchunguza Mielekeo ya Mioyo Yetu” kuelekea kuhudhuria mkutano. Msemaji-mwalikwa atatuonyesha jinsi ya “Kudumisha Hali ya Kiroho kwa Kujilisha Katika Meza ya Yehova.” Kitia-moyo kifaacho pia kitatolewa kwa vijana katika tengenezo la Yehova wadumishe uimara katika kumtumikia Mungu. Hotuba kuu ya msemaji-mwalikwa, yenye kichwa “Kuimarishwa Kiroho ili Kutoa Ushahidi Wenye Ujasiri,” itaonyesha jinsi maandalizi yaliyofanywa kupitia tengenezo yanavyotutayarisha tutoe ushahidi wenye ujasiri kuhusu Ufalme. Ni nani ambaye hangependa kunufaika na programu hii?
Watu wapya ambao wanataka kubatizwa wapaswa kujulisha mwangalizi-msimamizi upesi iwezekanavyo. Tuna uhakika kwamba tuanzapo mwaka wa 12 wa kusanyiko la pekee, kila mtu anayehudhuria ataimarishwa kiroho kwa ajili ya kazi iliyo mbele.