Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
‘Fanya Mambo Yote kwa Ajili ya Habari Njema,’ ndicho kichwa cha programu ya siku ya kusanyiko la pekee kuanzia Septemba. (1 Kor. 9:23) Habari ya Ufalme ni habari ya maana zaidi isikiwayo leo. Programu hiyo itatusaidia tuwe wabebaji wa habari hizi nzuri ajabu. Pia itatufanya tuwe jasiri tufulize kutangaza habari njema bila kuacha.—Mdo. 5:42.
Programu hiyo itatuonyesha jinsi ya kutumia mazoezi yetu ya kitheokrasi kikamili ili tuweze kutimiza mengi zaidi katika huduma. Tutasikia kutoka kwa wengine ambao wamefanya marekebisho ili kupanua utumishi wao, kutia na vijana ambao wanatoa waliyo nayo ili kuendeleza habari njema.—Linganisha Wafilipi 2:22.
Hotuba kuu, itakayotolewa na msemaji anayezuru, itakazia uhitaji wetu wa kudumu “kuwa twafaa kukabidhiwa habari njema.” (1 The. 2:4) Tutasaidiwa kuona kwamba ikiwa twapaswa kudumisha pendeleo letu la kushiriki habari njema na wengine, lazima tufikie matakwa ya Mungu na viwango katika kufikiri na mwenendo. Baraka tunazopokea kwa sababu ya kufanya hivi zitakaziwa pia.
Usikose programu hii muhimu. Wapya waliojiweka wakfu wanaotaka kubatizwa kwenye siku ya kusanyiko la pekee wapaswa kujulisha mwangalizi-msimamizi mara hii. Waalike wote ambao unajifunza nao wahudhurie. Na tumruhusu Yehova atuimarishe tufanye mambo yote kwa ajili ya habari njema na hivyo tutimize kazi iliyo kubwa zaidi kabla ya Har–Magedoni.