Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
1 Kwa nini tutangaze habari njema bila kuacha? Matakwa ya kuwa mhubiri wa habari njema ni yapi? Hata wale wenye haya na waoga wanawezaje kuchukua hatua ya kushiriki habari njema na wengine? Maswali haya na mengine yenye kuvuta fikira yatajibiwa katika programu ya siku ya kusanyiko la pekee ya mwaka wa utumishi wa 1996, iliyo na kichwa “Wenye Sifa ya Ustahili Kuwa Wahudumu wa Habari Njema.”—Linganisha 2 Wakorintho 3:5, NW.
2 Tukiwa watu wa Yehova, lazima tuwe waangalifu kuhusu tabia yetu. Mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo yatatolewa na vijana wanaosimulia jinsi walivyoshinda misongo ya marika. Wazazi wataandaliwa kitia-moyo chenye upendo kuhusu uhitaji wa kuzoeza watoto wao kuwa wahudumu wa Mungu. Sisi sote tutasaidiwa kuthamini uhitaji wa kuhubiri na baraka zitakazotujia sisi na wale wanaotusikiliza.—1 Tim. 4:16.
3 Kwa hakika ubatizo utakuwa jambo kuu la siku hiyo. Kabla ya tukio hili, hotuba inayotegemea Biblia itaelekezwa kwa watu waliojiweka wakfu hivi karibuni. Bila shaka, wote waliopo watataka kusikiliza kwa uangalifu habari ya ubatizo inapozungumzwa na maana yayo kueleweshwa wazi. Yeyote anayetaka kubatizwa kwenye siku ya kusanyiko la pekee apaswa kumjulisha mwangalizi-msimamizi mapema ili awe na wakati wa kutosha wa kupanga wazee wengine wapitie maswali yaliyochaguliwa pamoja na wataka-kubatizwa.
4 Jambo kuu jingine litakuwa hotuba ya msingi itakayotolewa na msemaji mwenye kuzuru. Ni yenye kichwa “Wenye Sifa ya Ustahili na Waliotayarishwa kwa Vifaa Kuwa Wahudumu wa Mungu.” Maandalizi manne makuu yanayotutayarisha tukiwa wahudumu yatazungumziwa, na hotuba itatia ndani mambo yaliyoonwa yenye kujenga imani.
5 Panga sasa ili uhudhurie programu nzima. Hakikisha umekaribisha watu wenye kupendezwa na wanafunzi wa Biblia ili kwamba pia waweze kunufaika na siku hii ya elimu ya kitheokrasi. Kwa njia hii twaweza kuhakikisha kwamba “tumekuwa wenye sifa ya ustahili” tukiwa wahudumu wa habari njema.