Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/98 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Januari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Januari
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Januari 5
  • Juma Linaloanza Januari 12
  • Juma Linaloanza Januari 19
  • Juma Linaloanza Januari 26
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 1/98 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Januari

Juma Linaloanza Januari 5

Wimbo 10

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.

Dak. 17: “Ona Upendezo Katika Kutoa Ushahidi Kamili.” Mazungumzo na wasikilizaji ya makala hiyo. Kazia mambo muhimu ya utoaji wenye matokeo: (1) Toa salamu ya kirafiki, (2) eleza au tokeza swali juu ya habari ya karibuni yenye kupendeza, (3) rejezea Andiko lifaalo, na (4) elekeza kupendezwa kwenye kichapo kinachotolewa. Panga uwe na mhubiri mwenye sifa ya ustahili atoe wonyesho wa utoaji wa mara ya kwanza na wa ziara ya kurudia inayolingana na huo.

Dak. 20: Jitayarishe Sasa Kutegemeza Sheria ya Mungu Kuhusu Damu. Mzee mwenye sifa ya ustahili azungumzia umaana wa kujaza kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia. Mwelekezo uliopuliziwa kwenye Zaburi 19:7 waonyesha kwamba Matendo 15:28, 29 ni wonyesho wa Mungu wa sheria kamilifu kuhusu damu. Waabudu waaminifu-washikamanifu hujitahidi kutegemeza sheria hiyo. Hati hii hujulisha azimio lako la kufanya hivyo na husema unapokuwa huwezi kujisemea mwenyewe. (Linganisha Mithali 22:3.) Kadi mpya huandaa tangazo la sasa la kukataa kwako kutiwa damu. Baada ya mkutano huu, Mashahidi waliobatizwa wanaotaka kuwa na kadi mpya watapewa hiyo, na wale walio na watoto wadogo watapokea Kadi ya Utambulishi kwa kila mtoto. Kadi hizi hazipasi kujazwa usiku huu. Zapasa kujazwa kwa uangalifu nyumbani lakini ZISITIWE sahihi. Kutia sahihi, kushuhudia, na kuandika tarehe za kadi zote kutafanywa baada ya Funzo la Kitabu la Kutaniko litakalofuata, chini ya usimamizi wa kiongozi wa funzo la kitabu. Kufanya hivyo kutahakikisha kwamba wote waliogawiwa kwenye kikundi chake wanaotaka kutekeleza mwelekezo huu wa kitiba wanapata msaada unaohitajika. Wale wanaotia sahihi wakiwa mashahidi kwa kweli wanapaswa kuona mwenye kadi akiitia sahihi hati hiyo. Mtu yeyote anayekosa wakati huo na anayetaka kujaza na kutia sahihi kadi atasaidiwa na viongozi/wazee kwenye Mkutano wa Utumishi utakaofuata hadi wahubiri wote waliobatizwa wawe wamemaliza kujaza kadi zao vizuri. (Pitia barua ya Oktoba 15, 1991.) Kwa kugeuza usemi ulio katika kadi hii kulingana na hali zao na masadikisho yao wenyewe, wahubiri wasiobatizwa wanaweza kuandika mwelekezo wao wenyewe wa kutumia na wa watoto wao.

Wimbo 142 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 12

Wimbo 125

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Eleza mipango ya pekee ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma.

Dak. 15: “Tumia Vizuri Vikaratasi vya Ukaribishaji.” Mazungumzo na wasikilizaji. Tia ndani jambo lililoonwa katika Mnara wa Mlinzi, Desemba 1, 1996, ukurasa wa 13, fungu la 15.

Dak. 20: “Yehova Hupa Nguvu Ipitayo Iliyo ya Kawaida.” Maswali na majibu. (Ona w90-SW 7/15 19, fungu la 15-16.) Panga wengine wasimulie mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo kuonyesha jinsi ambavyo Yehova amewatia nguvu.

Wimbo 81 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 19

Wimbo 1

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: Funzo la Familia Liletalo Shangwe. Wenzi waliooana wazungumzia mahitaji ya kiroho ya familia yao. Wakihangaishwa na mavutano ya kilimwengu yanayoathiri watoto wao vibaya, wanahisi uhitaji wa kutia nguvu hali ya kiroho ya watoto wao lakini wanatambua kwamba funzo lao la familia limekuwa likifanywa mara mojamoja na mara nyingi halina matokeo. Wakiwa pamoja, wanapitia mapendekezo ya jinsi ya kuongoza funzo la familia lenye maana yaliyotolewa katika Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 1997, ukurasa wa 26-29. Wote wawili wanaazimia kufuatia kulinda hali-njema ya kiroho ya watoto wao.

Wimbo 146 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 26

Wimbo 187

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Pitia toleo la fasihi la Februari. Taja jambo moja au mawili kutoka katika kitabu Upeo wa Ufunuo ambayo yatasaidia tunapokitoa.

Dak. 15: “Stahi Mahali pa Ibada pa Yehova.” Maswali na majibu. Ishughulikiwe na mzee, ambaye apaswa kutoa matumizi yenye fadhili ya kwenu.

Dak. 18: Kuripoti Fungu Letu Katika Kazi ya Kutoa Ushahidi ya Ulimwenguni Pote. (Ikitegemea kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 100-102, 106-110) Hotuba na mazungumzo yakishughulikiwa na mwandishi. Baada ya kuonyesha kielelezo cha Kimaandiko cha kuripoti utendaji wetu kwa ukawaida, anaalika watumishi wa huduma wawili wapitie kichwa kidogo “Sababu Inayotufanya Turipoti Utumishi wa Shambani Wetu.” Kisha mwandishi akazia umaana wa kuleta ripoti zilizo sahihi bila kukawia. Aeleza sababu kwa nini kuweka miradi ya kibinafsi kwanufaisha, akimalizia kwa maelezo yenye kutia moyo juu ya baraka wanazopata wale ambao wameshiriki kikamili katika kazi ya kutoa ushahidi.

Wimbo 189 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki