Tumia Vizuri Vikaratasi vya Ukaribishaji
1 Vikaratasi vya ukaribishaji vya kutaniko ni vyenye mafaa kwa kujulisha watu katika jumuiya anwani ya Jumba la Ufalme na saa zilizo sahihi za mikutano. Ingefaa kumwachia kila mtu unayekutana naye kimoja. Kwa kusudi hilo, kila kutaniko lapaswa kuweka vikaratasi vya ukaribishaji vya kutosha akibani. Kwa makutaniko ambayo hubadili saa za mikutano kila mwaka, Januari, vikaratasi vya ukaribishaji vipya vyapasa kuagizwa baada ya Oktoba kila mwaka ili vile vyenye saa mpya za mkutano vipatikane sikuzote. Fomu ya Agizo la Vikaratasi vya Ukaribishaji yapasa kutumiwa kwa kusudi hili. Unapokuwa navyo, vikaratasi vya ukaribishaji vyaweza kutumiwaje kwa manufaa?
2 Wahubiri wengi huona kwamba kumpa mtu kimoja ni njia yenye matokeo ya kujijulisha wenyewe na kuanzisha mazungumzo. Kueleza ratiba ya mkutano au ujumbe ulio upande ule mwingine kwaweza kufungua njia ya mazungumzo juu ya kazi yetu na kusudi lake. Wazazi wanaweza kuhusisha watoto wao wachanga katika huduma kwa kuwafanya watoe mlangoni kikaratasi cha kukaribisha watu. Wahubiri wanaoshiriki katika kutoa ushahidi wa kuandika barua wapaswa kuweka katika barua yao kikaratasi cha kukaribisha watu na kumwalika mtu ahudhurie mikutano. Huenda ikawa kwamba vikaratasi vya ukaribishaji vyaweza kuachwa kwenye nyumba zisizokuwa na watu, mradi kuwe na uangalifu wa kuviweka chini ya mlango ili viwe havionekani kabisa.
3 Vikaratasi vya ukaribishaji vimekuwa vikisaidia katika kuelekeza watu wenye mioyo ya kufuatia haki kwenye kweli. Jambo moja lililoonwa laeleza kuhusu mwanamke ambaye, kwa sababu ya kikaratasi cha kukaribisha watu, aliweza kutimiza tamaa yake ya muda mrefu ya kuelewa Biblia. Baada ya kusali usiku kucha kwa Mungu, wenzi waliooana walio Mashahidi walipiga kengele ya mlango wake asubuhi. Akitazama kupitia tundu la kuchungulia, alisema kwamba hangeweza kufungua mlango. Mashahidi hao walisukuma kikaratasi cha kukaribisha watu chini ya mlango. Kilisema hivi: “Ijue Biblia Yako.” Akakiona akafungua mlango. Funzo lilianzishwa mara hiyo, naye alibatizwa baadaye. Bila kudharau nguvu ya roho ya Mungu, na tutumie vizuri kwa ukawaida vikaratasi vya ukaribishaji tutimizapo kikamili huduma yetu.—Ona pia Huduma ya Ufalme Yetu ya Februari 1994, ukurasa wa 1.