Mpango Mpya wa Kupitia Programu za Makusanyiko
Ulimwengu wa Shetani unapozidi kuzorota, Yehova anatutia nguvu ili ‘tukatae kabisa kutomwogopa Mungu na tamaa za kilimwengu na tuishi kwa utimamu wa akili na uadilifu na ujitoaji-kimungu katikati ya mfumo wa mambo wa sasa.’ (Tito 2:12) Baadhi ya mipango ambayo anafanya kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ni makusanyiko ya mzunguko na makusanyiko ya pekee. (Mt. 24:45) Tunaimarishwa sana katika makusanyiko haya ya kiroho!
Ili tusaidiwe kutumia maishani mwetu mafundisho tunayopokea, tutatumia mpango mpya wa kupitia habari za makusanyiko hayo katika mwaka wa utumishi wa 2005. Katika ukurasa wa 5 na 6 wa nyongeza hii kuna makala zinazoonyesha mambo yatakayozungumziwa kwenye makusanyiko hayo na vilevile maswali ya kupitia programu za makusanyiko hayo. Makutaniko yatazungumzia habari hizo kwenye Mkutano wa Utumishi muda mfupi kabla na baada ya kuhudhuria makusanyiko yao. Mapitio hayo yatapangwaje?
Juma moja au mawili kabla kutaniko halijahudhuria kusanyiko la mzunguko, hotuba ya dakika kumi inayotegemea makala “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko” itatolewa kwenye Mkutano wa Utumishi ili kuwatia ndugu hamu ya kusikiliza programu. Msemaji atataja pia maswali ya kupitia na kuwatia wote moyo waandike mambo makuu ili wawe tayari kwa ajili ya pitio litakalofanywa majuma machache baada ya kusanyiko.
Majuma machache baada ya kusanyiko, muda wa dakika 15 utatumiwa kupitia programu ya siku ya kwanza ya kusanyiko katika Mkutano wa Utumishi. Juma linalofuata, dakika 15 zitatumiwa kupitia programu ya siku ya pili ya kusanyiko. Mazungumzo hayo yatategemea maswali ya kupitia yanayopatikana katika nyongeza hii. Pitio hilo linapaswa kukazia hasa jinsi tunavyoweza kutumia habari hizo maishani mwetu. Ili kupata nafasi ya kufanya mapitio hayo, wazee wanapaswa kufupisha au kufuta sehemu nyingine za Mkutano wa Utumishi, au kupanga zishughulikiwe juma lingine.
Pitio la programu ya kusanyiko la pekee linapaswa kufanywa kwa njia iyo hiyo, lakini programu nzima itapitiwa katika pindi moja tu ya dakika 15. Kila mmoja wetu anapaswa kuhifadhi nyongeza hii na kuitumia ili kunufaika kikamili na mafundisho mazuri ambayo Yehova hutuandalia.—Isa. 48:17, 18.