Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/04 uku. 5
  • Pitio La Kusanyiko La Mzunguko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio La Kusanyiko La Mzunguko
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Pitio La Kusanyiko La Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Mpango Mpya wa Kupitia Programu za Makusanyiko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Pitio la Kusanyiko la Mzunguko
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 8/04 uku. 5

Pitio La Kusanyiko La Mzunguko

Makala hii itatumiwa kupitia programu ya kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi wa 2005, kabla na baada ya kusanyiko. Makala yenye kichwa, “Mpango Mpya wa Kupitia Programu za Makusanyiko,” kwenye ukurasa wa 4 katika nyongeza hii, inaeleza jinsi ya kufanya mapitio hayo. Maswali yote yanapaswa kuzungumziwa wakati wa pitio litakalofanywa baada ya kusanyiko. Pitio linapaswa kukazia jinsi tunavyoweza kutumia maishani mwetu mambo tuliyojifunza kusanyikoni.

KIPINDI CHA ASUBUHI SIKU YA KWANZA

1. Ni nini kitakachotusaidia kupata hekima ya Mungu?

2. Ndugu na dada katika mzunguko wamefanya jitihada gani ili kuwapata watu wengi zaidi ili wawahubirie habari njema?

KIPINDI CHA ALASIRI SIKU YA KWANZA

3. Kwa nini ni muhimu kwa Mkristo awe safi kiakili na kiroho? Tunaweza kufaulu jinsi gani kuwa safi kiakili na kiroho?

4. Tunaweza kujionyesha kuwa wenye kufanya amani jinsi gani tunaposhirikiana na ndugu zetu?

5. Usawaziko ni nini, na tunawezaje kuonyesha sifa hiyo tunapotenga wakati ili tutimize wajibu mbalimbali?

6. Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Sauli na Noa? Tunaweza kuonyesha kwa njia zipi kwamba sisi tuko “tayari kutii”? (Yakobo 3:17)

7. Wakristo wanaweza kujihadhari jinsi gani wasiishi maisha maradufu?

8. Tunawezaje kusema hekima ya Mungu kama Paulo?

KIPINDI CHA ASUBUHI SIKU YA PILI

9. Kwa nini tunapaswa kuchagua mambo tunayotaka kufuatia kwa busara, na ni nini kitakachotusaidia kufanya maamuzi mazuri?

10. Ndugu na dada katika mzunguko wanafanya jitihada gani ili kuhudhuria mikutano kwa ukawaida, nao wamenufaikaje kwa kufanya hivyo?

11. Vichwa wa familia wanawezaje kuwaimarisha kiroho watu wa familia zao?

12. Tuliarifiwa kuhusu mahitaji gani ya mzunguko?

KIPINDI CHA ALASIRI SIKU YA PILI

13. Kama hotuba ya watu wote ilivyoonyesha, hekima kutoka juu imechochea matendo gani ya uadilifu?

14. Kwa nini ni upumbavu kujitegemea au kuwategemea wale wasioongozwa na hekima ya Mungu? Sisi tunapaswa kujihadhari kuhusiana na mambo gani?

15. Hekima ya Mungu hutulinda na mitego gani?

16. Kwa nini ni muhimu kwetu kufuata ushauri tuliopokea kwenye kusanyiko la mzunguko?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki