Pitio la Kusanyiko la Mzunguko
Habari hii itapitiwa katika Mkutano wa Utumishi muda mfupi kabla na baada ya kutaniko kuhudhuria kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi wa 2006. Mwangalizi msimamizi atapanga sehemu hizi za pitio kulingana na maagizo yaliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 2004, ukurasa wa 4. Maswali yote yanapaswa kuzungumziwa wakati wa pitio. Mnapaswa kukazia jinsi tunavyoweza kutumia habari iliyotolewa kusanyikoni.
SIKU YA KWANZA
1. Tunavaaje utu mpya, na kwa nini tunapaswa kuudumisha?
2. Wahubiri fulani wameongezaje wakati wanaotumia katika kazi ya kuhubiri?
3. Kwa nini hatupaswi kujilinganisha na wengine?
4. Washiriki wa familia wanawezaje kuonyesha utu mpya katika familia?
5. Tunawezaje kuliunga kutaniko mkono kwa ushikamanifu?
6. Kwa nini tunahitaji kuonyesha utu mpya tunapohubiri?
7. Kutafakari kwa njia inayofaa kunatia ndani nini, na tunafaidikaje tukitafakari kwa njia hiyo?
8. Yehova anaweza kutufinyanga tukiwa na sifa gani?
SIKU YA PILI
9. Ni muhimu kadiri gani kutumia ulimi wetu ipasavyo?
10. Kuna faida gani kutumia usemi unaofaa tunapochangamana na wafanyakazi wenzetu, wanashule wenzetu, na wengine?
11. Tunawezaje kutumia shauri la Paulo katika Waefeso 4:25-32 tunaposhughulika na waamini wenzetu?
12. Tunaweza kutumia ulimi wetu kwa heshima zaidi katika njia gani?
13. Ni lazima tufanye nini ili tumshinde yule mwovu?
14. Tunapaswa kujitahidi kuwa bila doa kutokana na ulimwengu katika mambo gani?
15. Kwa nini tunapaswa kumfanya upya mtu tuliye kwa ndani siku baada ya siku, na tunawezaje kufanya hivyo?
16. Unapanga kutumia shauri gani ambalo umepata katika kusanyiko la mzunguko la mwaka huu?