Pitio la Kusanyiko la Pekee
Habari hii itapitiwa katika Mkutano wa Utumishi muda mfupi kabla na baada ya kutaniko kuhudhuria kusanyiko la pekee la mwaka wa utumishi wa 2006. Mwangalizi msimamizi atapanga sehemu hizi za pitio kulingana na maagizo yaliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 2004, ukurasa wa 4. Maswali yote yanapaswa kuzungumziwa wakati wa pitio na kukazia jinsi tunavyoweza kutumia habari hiyo maishani mwetu.
KIPINDI CHA ASUBUHI
1. Inamaanisha nini kuwa na jicho rahisi, na kwa nini ni vigumu kuwa na jicho rahisi leo? (“Kwa Nini Uwe na Jicho Rahisi?”)
2. Tunapata faida gani tukiwa na jicho rahisi? (“Pata Baraka za Kuwa na Jicho Rahisi”)
3. Ni hatari zipi zinazotokana na mambo yanayosemekana ni ya kawaida tu? (“Kuwa na Jicho Rahisi Katika Ulimwengu Mwovu”)
KIPINDI CHA ALASIRI
4. Wazazi na wengine wanawezaje kuwatia moyo vijana wafuatie miradi ya kiroho? (“Wazazi Wanaolenga Mishale Yao Vizuri” na “Vijana Wanaofuatia Miradi ya Kiroho”)
5. Tunawezaje kusonga mbele pamoja na tengenezo la Yehova (a) tukiwa mtu mmoja-mmoja? (b) tukiwa familia? (c) tukiwa kutaniko? (“Zingatia Kusonga Mbele Pamoja na Tengenezo la Yehova”)