Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/04 uku. 5
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Pitio La Kusanyiko La Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Kusanyiko la Mzunguko Litakalotusaidia Kulinda Hali Yetu ya Kiroho
    Huduma ya Ufalme—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 8/04 uku. 5

Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko

Katika ‘nyakati hizi za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,’ tunahitaji hekima ya Mungu ili kupata na kudumisha kibali cha Yehova. (2 Tim. 3:1) Tutapata ushauri na kutiwa moyo kwenye kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi wa 2005 wakati kichwa, “Ongozweni na ‘Hekima Inayotoka Juu’” kitakapozungumziwa katika hotuba mbalimbali.—Yak. 3:17.

Mfululizo wa kwanza wa hotuba, “Kuonyesha ‘Hekima Inayotoka Juu’ Maishani Mwetu,” utatusaidia kuona maana ya kuwa safi kiadili, mwenye kufanya amani, mwenye usawaziko, na tayari kutii. Kisha mwangalizi wa mzunguko atazungumzia sehemu nyingine tatu za hekima ya Mungu. Mwangalizi wa wilaya atamalizia siku ya kwanza kwa kuonyesha jinsi wahudumu Wakristo wanavyoelimishwa kusema hekima ya Mungu, ijapokuwa watu fulani huwaona kuwa watu “wasio na elimu na wa kawaida.”—Mdo. 4:13.

Katika siku ya pili, mfululizo wa hotuba wenye kichwa, “Fuatia Mambo Yanayojenga,” utatusaidia kutambua na kuepuka mambo yanayotudhoofisha kiroho. Mfululizo huo utatuonyesha pia jinsi tunavyoweza kuwajenga wengine kwenye mikutano ya kutaniko, katika huduma ya shambani, na nyumbani. Hotuba ya watu wote yenye kichwa, “Jinsi Hekima ya Mungu Inavyotunufaisha,” itatusaidia kuthamini zaidi manufaa tunayopata kwa kufuata kanuni za Mungu maishani mwetu. Hotuba ya mwisho yenye kichwa, “Kutenda Kulingana na Hekima ya Mungu Hutulinda,” itatuimarisha kushikilia azimio letu la kumwendea Yehova ili tupate hekima katika siku hizi za mwisho.

Ubatizo wa wanafunzi wapya ni jambo muhimu kwenye kila kusanyiko. Kusanyikoni tutapata pia Shule ya Kitheokrasi na Funzo la Mnara wa Mlinzi la juma lile. Yehova anataka sisi sote tunufaike na hekima anayotoa. Tutafaidika sana kiroho kwa ushauri na mambo yenye kutia moyo tutakayopata kwenye kusanyiko letu la mzunguko.—Met. 3:13-18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki