Pitio La Kusanyiko La Pekee
Makala hii itatumiwa kupitia programu ya kusanyiko la pekee la mwaka wa utumishi wa 2005, kabla na baada ya kusanyiko. Makala yenye kichwa, “Mpango Mpya wa Kupitia Programu za Makusanyiko,” kwenye ukurasa wa 4 wa nyongeza hii, inaeleza jinsi ya kufanya mapitio hayo. Maswali yote yanapaswa kuzungumziwa wakati wa pitio litakalofanywa baada ya kusanyiko. Pitio hilo linapaswa kukazia jinsi tunavyoweza kutumia maishani mwetu mambo tuliyojifunza kusanyikoni.
KIPINDI CHA ASUBUHI
1. Kwa nini umuhimu wa kumsikiliza Yehova unazidi daima? Kusikiliza kunamaanisha nini? (“Kwa Nini Tusikilize Sauti ya Yehova?”)
2. Familia zinawezaje kudumisha mpango mzuri wa utendaji wa kiroho? (“Familia Zinazosikiliza Neno la Mungu Bila Kukengeushwa”)
3. Ndugu na dada katika mzunguko wametumiaje fursa mbalimbali za kutoa ushahidi? (“Kufanya Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu”)
4. Tunapata masomo na onyo gani tunaposoma Waebrania sura ya 3 na 4? Yehova anasema nasi kwa njia gani leo? (“Kusikiliza Mungu Anaposema Hutulinda”)
5. Hotuba ya ubatizo ilikunufaishaje? (“Wakfu na Ubatizo”)
KIPINDI CHA ALASIRI
6. Tunatambua jambo gani kuhusu Yesu alipokuwa kijana, na vijana katika mzunguko wanaigaje mfano wake? (“Jinsi Kusikiliza Neno la Mungu kwa Makini Kunavyowaimarisha Vijana Wetu”)
7. Wazazi wanaweza kutumia njia zipi kuwazoeza watoto wao wachanga na wadogo kufuata njia za Yehova? (“Watoto Wachanga Wanaomsikiliza Mungu na Kujifunza”)
8. Tunapaswa kumsikiliza Yehova, Mwanawe, na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” kuhusiana na mambo gani hasa? (Mt. 24:45) Kwa nini ni muhimu sana kuyazingatia mambo hayo? (“Sikiliza Daima Mafundisho ya Mungu”)