Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/13 uku. 1
  • Neno la Mungu Ni Lenye Faida kwa Kufundisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Neno la Mungu Ni Lenye Faida kwa Kufundisha
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Furahia Manufaa za Ufundishaji wa Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Linda Akili Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • ‘Mapenzi ya Mungu na Yatendeke’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 8/13 uku. 1

Neno la Mungu Ni Lenye Faida kwa Kufundisha

1. Programu ya kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi wa 2014 ina kichwa gani, na ni swali gani litakalojibiwa?

1 ‘Mfundishaji wetu Mkuu,’ Yehova, ndiye mwalimu bora zaidi! (Isa. 30:20, 21) Lakini Yehova anatufundishaje? Ametupatia kitabu kisichoweza kulinganishwa na vitabu vingine. Kitabu hicho kilichoongozwa na roho ni Biblia. Neno la Mungu linaweza kutusaidiaje kimwili, kiakili, kihisia, na kiroho? Jibu la swali hilo litazungumziwa katika kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi wa 2014. Kichwa cha kusanyiko hilo ni, “Neno la Mungu Ni Lenye Faida kwa Kufundisha,” kinachotegemea andiko la 2 Timotheo 3:16.

2. Ni maswali gani yatakayotusaidia kujua mambo makuu?

2 Tafuta Mambo Makuu Yafuatayo: Majibu ya maswali yafuatayo ndiyo mambo makuu yatakayozungumziwa katika kusanyiko hilo:

• Mafundisho ya Mungu yana faida gani maishani mwetu? (Isa. 48:17, 18)

• Yehova anatuhakikishia nini ikiwa tutarekebisha hali zetu ili tumtumikie wakati wote? (Mal. 3:10)

• Tunapaswa kutendaje tunapopata “mafundisho mageni”? (Ebr. 13:9)

• Tunawezaje kuiga ‘njia ya Yesu ya kufundisha’? (Mt. 7:28, 29)

• Kwa nini wale wanaofundisha kutanikoni wanapaswa kwanza wajifundishe wenyewe? (Rom. 2:21)

• Neno la Mungu lina faida gani? (2 Tim. 3:16)

• Watu wanafaidikaje kutokana na ‘kutikiswa’ kwa mataifa? (Hag. 2:6, 7)

• Yehova ana uhakika gani kuhusu watumishi wake? (Efe. 5:1)

• Kwa nini tunapaswa kujitahidi kuendelea kutumia mambo tunayojifunza kutoka kwa Yehova? (Luka 13:24)

3. Kwa nini ni muhimu tuhudhurie na kusikiliza kwa makini kusanyiko hilo lililotayarishwa kwa wakati unaofaa?

3 Mwanzoni mwa andiko la 2 Timotheo sura ya 3, kabla tu ya kuandika maneno yanayotegemeza kichwa cha kusanyiko tutakalohudhuria, Paulo alieleza kuhusu hali ngumu za siku za mwisho. Aliandika hivi: “Watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mpaka ubaya zaidi, wakipotosha na kupotoshwa.” (2 Tim. 3:13) Ili tusipotoshwe ni muhimu tusikilize na kutumia mambo tunayojifunza kutoka kwa Yehova! Kwa hiyo, na tuazimie kuhudhuria na kusikiliza kwa makini kusanyiko hilo lililotayarishwa kwa wakati unaofaa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki