Huduma ya Ufalme Yetu Yapata Umbo Jipya
Kuanzia na toleo la Septemba Huduma ya Ufalme Yetu inatokea ikiwa na umbo jipya. Muundo huo ulio bora zaidi utarahisisha mipangilio ya kazi ya kutokeza kichapo hiki cha kila mwezi kwa lugha nyingi na kuifanya iwe rahisi kwa wasomaji kupata habari maalumu wanayotafuta.
Katika umbo hili jipya, vichwa vyote vya habari na maandishi yaweza kutokezwa na kompyuta, hivyo kuondolea mbali uhitaji wa kubandika kwa mkono vikaratasi vyenye vichwa vya habari. Jambo hilo larahisisha sana kazi ya kuchapa Huduma ya Ufalme Yetu.
Kwa msomaji, kuna mambo mbalimbali yaliyofanyiwa maendeleo. Kuna upatano wa ukubwa wa chapa, na sura ya chapa iliyochaguliwa kwa ajili ya maandishi inasomeka vizuri sana, hata katika ukubwa mdogo. Ripoti ya utumishi wa shambani itakuwa rahisi kusomeka. Pia, makala kuu zitatokea kwa ukawaida katika kurasa za nje, na makala zilizo nyingi zitamaliziwa kwenye ukurasa ule ule mmoja. Programu ya Mikutano ya Utumishi, ratiba ya Funzo la Kitabu la Kundi, ripoti ya utumishi, Matangazo, Habari za Kitheokrasi, Mikutano ya Utumishi wa Shambani, Kichwa cha Mazungumzo, na Sanduku la Swali zitapatikana katika kurasa za ndani.
Twatumaini kwamba utaona kifaa hiki kuwa chenye kuvutia zaidi na kuwa msaada wenye mafanikio katika kazi ya kuhubiri habari njema za Ufalme na kufanya wanafunzi.