Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/91 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Septemba 2
  • Juma Linaloanza Septemba 9
  • Juma Linaloanza Septemba 16
  • Juma Linaloanza Septemba 23
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 9/91 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba

Juma Linaloanza Septemba 2

Wimbo 17

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Kazia mambo makuu ya kuzungumzia kutoka matoleo ya karibuni ya magazeti.

Dak. 20: “Kutoa Habari Njema—Kuanza Mafunzo kwa Njia ya Moja kwa Moja.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Baada ya kuzungumza fungu la 3 na la 4, toa wonyesho wa kutumia njia ya moja kwa moja kwa kutumia kitabu Kuishi Milele. na trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani. Njia ya moja kwa moja itakusaidia kuamua kadiri ya kupendezwa kwa mwenye nyumba. Kazia uhitaji wa kurudia kupendezwa kote iwe fasihi imeangushwa katika ziara ya kwanza au la. Watie moyo wote wajaribu kuanza mafunzo ya Biblia kwa kutumia njia ya moja kwa moja katika utumishi wa shambani mwishoni mwa juma hili.

Dak. 15: Sanduku la Swali. “Huduma ya Ufalme Yetu Yapata Umbo Jipya,” na Habari za Kitheokrasi. Watie moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani mwishoni mwa juma hili.

Wimbo 157 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 9

Wimbo 214

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo katika magazeti ambayo yatatumiwa katika utumishi wa shambani mwishoni mwa juma hili. Kuwe na wonyesho wa utoaji mmoja au mawili kadiri wakati uruhusuvyo.

Dak. 20: Jiwekee Miradi ya Kibinafsi kwa Mwaka Huu Mpya wa Utumishi. Mwangalizi wa utumishi apitie utendaji wa kundi kwa mwaka wa utumishi uliopita. Pongeza kwa uchangamfu pande zinazoonyesha maendeleo. Eleza maeneo yanayohitaji kuelekezewa fikira zaidi katika kundi lenu wakati wa mwaka mpya wa utumishi, kama vile kueneza eneo, wahubiri na mapainia kuwa na maeneo yao wenyewe, kusaidia vijana wafanye maendeleo ya kiroho, halafu toa madokezo. Pitia ripoti ya mwisho ya mwangalizi wa mzunguko. Tumia Index ili kupata habari juu ya uhitaji na jinsi ya kutumia ushauri uliotolewa. Wale wanaovumilia katika utumishi wa uaminifu hutia moyo wengine. (Ebr. 6:10) Hoji wahubiri wawili au mapainia ambao walifanya maendeleo katika mwaka wa utumishi uliopita. Wamejiwekea miradi gani kwa mwaka wa 1992? Pia, hoji mhubiri au painia ambaye ametumika miaka mingi, aeleze magumu aliyopata na jinsi alivyoyashinda kwa msaada wa Yehova na tengenezo lake. Watie moyo wote wajiwekee miradi inayofaa ili kufanyia maendeleo huduma yao katika mwaka wa utumishi wa 1992.

Dak. 15: “Kutwaa Daraka Letu Tufanye Mema kwa Wengine.” Utoaji wa maswali na majibu. Wakati wa kuzungumzia fungu la 4, onyesha jinsi mzee kwenye Jumba la Ufalme awezavyo kumpongeza mhubiri kwa kielelezo chake bora cha uaminifu kwa muda wa miaka iliyopita. Aweza kuuliza ni jambo gani linaloweza kufanywa ili kumsaidia. Hata hivyo, mkazo wapasa kuwekwa juu ya pongezi.

Wimbo 94 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 16

Wimbo 44

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu. Soma shukrani kutoka kwa Sosaiti kwa ajili ya michango iliyopelekwa na kueleza uthamini kwa utegemezo wa kifedha kwa utendaji wa Sosaiti pamoja na ule wa kundi.

Dak. 20: “Mpango wa Funzo la Kitabu la Kundi—Sehemu ya 3.” Viongozi wawili wa Funzo la Kitabu la Kundi wazungumze habari, waitumie ihusu kundi lenu. Kazia faida wanazopata wote wakati wahubiri wanaposhirikiana na mipango ya utumishi. Taja uhitaji wa kuonyesha staha kwa nyumba zinazotumiwa wakati wa kukutana kwa ajili ya utumishi wa shambani, na kuwasifu wale ambao kwa kuonyesha ukaribishaji-wageni huruhusu nyumba zao zitumiwe. (km-SW 4/86 uku. 3) Kwa kuwa mahali pengine panahitajiwa pindi kwa pindi, yeyote anayetaka kutoa nyumba yake itumiwe aweza kumwambia mwangalizi msimamizi au mwangalizi wa utumishi. Funganisha na mambo kutoka mazungumzo ya juma lililopita juu ya kujiwekea miradi ya utumishi. Mwangalizi wa utumishi aweza kusaidia na kutia moyo wahubiri watimize miradi katika huduma.

Dak. 15: “Vijana—Je! Mtaupita Mtihani wa Uaminifu-Mshikamanifu wa Kikristo?” Hotuba ikitegemea makala katika Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 1991. Kazia upumbavu wa kuishi maisha ya aina mbili.

Wimbo 171 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 23

Wimbo 187

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kazia jambo moja au mawili kutoka katika magazeti ya karibuni. Watie moyo wahubiri washiriki katika utumishi wa shambani mwishoni mwa juma hili.

Dak. 20: “Uwe Mwenye Nafsi Yote Katika Huduma ya Shambani—Sehemu ya 3.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Katika fungu la 4, mhubiri mwenye ujuzi atoe wonyesho wa jinsi ya kusaidia mhubiri mpya zaidi wanapokuwa nje katika utumishi. Onyesha vipindi vya mazoezi huku mhubiri mpya akitumia madokezo ya mhubiri mwenye ujuzi kushinda vipingamizi vinavyotokea kikweli.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu au mazungumzo ya tangulizi zinazofaa kutumiwa katika eneo lenu. Mazungumzo yategemee kitabu Kutoa Sababu, kurasa 9-15. Waweza kusimulia kifupi mambo yaliyoonwa na wahubiri ambao wameanza mafunzo ya Biblia mwezi huu kwa kutumia njia ya moja kwa moja.

Wimbo 70 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki