Wimbo 157
Mwabudu Yehova Wakati wa Ujana
1. Watoto kasifu Mungu kale;
Wakapa Yesu vigelegele.
Wanaweza kutukuza Mungu,
Na wazee kutakasa Mungu.
2. Wazazi munaopenda kweli,
Mu wa Mungu mawakili ili
Mufunze watoto kucha Mungu.
Watoto watiini wazazi.
3. Vijana, muwe safi mwendoni;
Jifunze kutegemea Mungu.
Musitafute sifa ya watu,
Rafiki wabaya huharibu.
4. Ujanani Mungu mukumbuke,
Kwa roho, kweli mutumikie,
Mutakuja kufurahi sana,
Mufurahishe moyo wa Mungu.