Uwe Mwenye Nafsi Yote Katika Huduma ya Shambani
Sehemu ya 4: Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu kwa Mafanikio
1 Huduma ya waziwazi ya nafsi yote hutaka mpango mzuri wa kibinafsi. Yesu aliweka kigezo chenye kutokeza kwa utendaji wetu wa huduma leo. (Lk. 10:1, 2; Mdo. 1:8) Tunaweza kujifunza pia kutokana na njia ambayo wanafunzi wake wa karne ya kwanza walivyotimiza huduma yao. (Mdo. 5:42; 2 Tim. 4:5) Lakini ni jinsi gani unavyoweza kuwa na mipango mizuri zaidi na kufurahia matokeo mazuri kama hayo leo?
2 Ratibu Wakati kwa Utumishi wa Shambani: Huduma yetu si upande wa vivi hivi au wa kushtukia tu wa maisha yetu. Kiasi cha wakati tutumiacho kutimiza huduma yetu hakiwezi kuachwa kitukie kwa nasibu. Ili kupangia huduma yetu kwa mafanikio, ni lazima tutenge wakati kwa zile sehemu mbalimbali zayo. (Efe. 5:15, 16) Wahubiri wengi hulipata kuwa jambo lenye kusaidia kuweka mradi kuhusu ni saa ngapi watakazotumia katika huduma kila mwezi. Kwa kawaida hiyo hutaka wapange mambo yao ili washiriki katika utumishi wa shambani kila juma. Wazazi Wakristo wapaswa kusaidia watoto wao waratibu wakati wa kushiriki kwa ukawaida katika sehemu mbalimbali za huduma ya shambani.—Kum. 6:7; Mit. 22:6.
3 Weka Miradi Yenye Maana: Miradi inayoweza kutimizwa itakupa jambo la kulenga. Mradi wako utimizwapo, utapata furaha ya kujisikia umetimiza jambo. (Mit. 13:12) Mtume Paulo alihimiza hivi: “Kwa vyovyote, kwa kadiri tulivyofanya maendeleo, na tuendelee kutembea kwa utaratibu katika kawaida ii hii.” (Flp. 3:16, NW) Kama ilivyo kwa pande zote za maendeleo yetu ya kiroho, utendaji wako wa shambani wapasa kutoa ushuhuda wa kawaida yenye utaratibu.
4 Kwa mfano, je, una kiasi cha kutosha cha trakti na vikaratasi vya kukaribisha watu kwenye mikutano? Je! Unaweka kiasi cha kutosha cha magazeti ya karibuni, na je, yako katika hali nzuri? Je! unatumia vizuri vikaratasi vya maandishi ya nyumba kwa nyumba, ukitumia kimoja kuandika kupendezwa na kingine wasiokuwamo nyumbani?
5 Kabla ya kushiriki huduma, tumia wakati kurudia Kichwa cha Mazungumzo cha wakati huu. Tenga mambo ya kuzungumzia katika kichapo kinachotolewa, na kuwa tayari kuyatumia ili kuchochea kupendezwa. Pia, uwe tayari kutumia kitabu cha marejezo cha utumishi wa shambani Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko. Hata katikati ya ziara, unaweza kurejezea upesi baadhi ya madokezo yacho mengi. Kutumia mambo hayo yenye kuleta matokeo kutafanyia maendeleo kufanikiwa kwa huduma yako.
6 Kuwa na ushiriki kamili katika “kazi takatifu ya habari njema” wakati wa hizi siku za mwisho ni pendeleo lenye baraka. (Rum. 15:16, NW) Twapaswa kujitahidi kutimiza huduma yetu kwa kutoa ushahidi bora zaidi iwezekanavyo, “tunda la midomo” (Ebr. 13:15; linganisha Hosea 14:2.) Ili kufanya hivyo, acheni turatibu wakati kwa ushiriki wa ukawaida katika utumishi wa shambani na kuweka miradi inayoweza kutimizwa ambayo itatuwezesha kutimiza huduma yetu kwa sifa ya Yehova.