Mikutano ya Utumishi kwa Oktoba
TAARIFA: Huduma ya Ufalme Yetu itaratibu Mikutano ya Utumishi kwa kila juma wakati pindi ya mkusanyiko. Makundi yanaweza kufanya marekebisho kama inavyohitajiwa ili kuruhusu wakati wa kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya halafu kuwe na pitio la dakika 30 kuhusu mambo makuu ya programu kwenye Mkutano wa Utumishi juma linalofuata. Pitio la siku baada ya siku laweza kugawiwa mapema ndugu wawili au watatu wanaostahili ambao wataweza kukazia mambo ya msingi. Pitio hilo lililotayarishwa vizuri litasaidia akina ndugu kukumbuka mambo ya msingi ili wayatumie kibinafsi na shambani. Maelezo kutoka kwa wasikilizaji na mambo yaliyoonwa yanayosimuliwa yapaswa kuwa mafupi na kutokeza wazo kuu.
Juma Linaloanza Septemba 30
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma ya Ufalme Yetu. Taja kifupi mambo ya kuzungumziwa katika magazeti ambayo yaweza kutumiwa mwisho wa juma hili.
Dak. 20: “Kufahamu Umaana wa Matukio ya Wakati Huu.” Maswali na majibu. Baada ya kuzungumza fungu la 6, toa wonyesho kwa kutumia Kichwa cha Mazungumzo. Tumia habari hususa katika gazeti Amkeni! la karibuni.
Dak. 15: Jinsi ambavyo gazeti Amkeni! limetufaidi sisi binafsi. Ndugu anayestahili awahoji wahubiri watatu au wanne. Tia ndani angalau kijana mmoja wa umri wa kwenda shule.
Wimbo 174 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 7
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Uwe Mwenye Nafsi Yote Katika Huduma ya Shambani—Sehemu ya 4.” Hotuba. Watie moyo vichwa vya familia wasaidie wote katika familia wajifanyie mipango na kujiwekea miradi ya utumishi wanayoweza kutimiza.
Dak. 15: “Kutoa Habari Njema—Kwa Kutumia Vichapo kwa Hekima.” Maswali na majibu. Tumia habari ihusu kundi lenu.
Dak. 10: “Kwa Nini Kujivika Unyenyekevu?” Hotuba yenye kutia moyo ikitegemea makala katika Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1991, kurasa 27-30.
Wimbo 92 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 14
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi, ripoti ya hesabu. Shukrani kwa ajili ya upaji. Lijulishe kundi ripoti ya utumishi wa shambani kwa mwezi Septemba.
Dak. 20: “Panga Sasa Kuhudhuria ‘Wapendao Uhuru’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1991”—Sehemu 1. Mazungumzo ya mafungu 1-9 pamoja na wasikilizaji, na pitio fupi juu “Vikumbusho vya Mkusanyiko wa Wilaya” kadiri wakati uruhusuvyo. Huenda wahubiri wakataka kuzungumza mambo yafaayo na wanafunzi wa Biblia wao watakaohudhuria mkusanyiko.
Dak. 15: “Vijana Wakristo—Iweni Imara katika Imani.” Mazungumzo ya familia, yakitegemea makala katika Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1991, kurasa 23-6. Baba aongoza mazungumzo yanayotia ndani mke na watoto. Teua njia ambazo katika hizo vijana waweza kukabili kwa mafanikio majaribu mbalimbali ya imani shuleni.
Wimbo 183 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 21
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 18: “Mpango wa Funzo la Kitabu la Kundi—Sehemu ya 4.” Maswali na majibu. Kazia uhitaji wa wote kupendezwa kibinafsi na mmoja na mwenzake katika kikundi cha funzo la kitabu.
Dak. 22: “Panga Sasa Kuhudhuria ‘Wapendao Uhuru’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1991”—Sehemu ya 2. Mazungumzo ya mafungu 10-22 pamoja na wasikilizaji. Tia ndani vikumbusho vifaavyo vikitegemea habari katika Mnara wa Mlinzi wa June 15, 1989, kurasa 10-20. Tia moyo vikundi vya familia vipitie mambo katika makala hizo kabla ya kuhudhuria mkusanyiko.
Wimbo 116 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzia kifupi toleo la mwezi wa Novemba.
Dak. 20: Kutafuta na Kufundisha Wastahilio. Hotuba na mahoji. Kazia Mathayo 10:11. Kupata watu nyumbani ni tatizo linalozidi kuongezeka nalo linaweza kuwa na matokeo dhahiri juu ya matokeo ya kazi na shangwe yetu. Ni jambo gani linaloweza kufanywa? (km-SW 7/85 uku. 4) Waendee watu katika nyua zao. Weka maandishi ya wale wasiokuwamo nyumbani na kurudia bila kukawia. Wengine wamekuwa na mafanikio mazuri kwa kupata watu kama hao nyumbani jioni, hivyo shiriki kazi ya kutoa ushahidi jioni. (km-SW 6/87 uku. 4) (Hoji kifupi wahubiri na/au painia wawili au watatu ambao wamekuwa na mafanikio katika kazi ya kutoa ushahidi jioni.) Shetani atatumia njia yoyote iwezekanayo kutuzuia tusipate watu wastahilio. Lazima tuwatafute. “Kondoo” ni wa Yesu Kristo. Ametuamuru tuwapate na kuwalisha. (Yn. 21:15-17) Jambo hilo latusaidia kuthamini uhitaji wa kufikia wakaaji wa kila nyumba ikiwezekana.
Dak. 15: “Kujenga Nyutu za Kikristo Katika Watoto Wetu.” Mazungumzo ya ndugu wawili juu ya makala katika Mnara wa Mlinzi wa Julai 1,1991, kurasa 24-27. Kazia uhitaji wa jitihada za bidii upande wa wazazi. Tumia habari ihusu mahitaji ya kundi lenu.
Wimbo 18 na sala ya kumalizia.