Matangazo
◼ Toleo la fasihi kwa Desemba: Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Januari na Februari: Kitabu chochote cha kurasa 192 kilichochapishwa katika 1983 au mapema zaidi. Ikiwa kundi halina akiba ya vitabu hivyo, kitabu Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani,” kitolewe na chaweza kuagizwa kutoka ofisi ya tawi. Machi: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
◼ Mwangalizi msimamizi au mtu yeyote aliyepewa mgawo naye apaswa kukagua hesabu ya kundi Desemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo.
◼ Makundi yapaswa kuanza kuagiza mabuku yaliyojalidiwa ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ya 1991 katika agizo lao la fasihi la Desemba. Mabuku hayo yatapatikana katika Kiingereza na Kifaransa. Mabuku hayo yaliyojalidiwa huwa ni vifaa vya kuagizwa kwa kiasi.—Ona Orodha ya Bei, mafungu 10-12.
◼ Marekebisho katika kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!:
Ukurasa 182, safu 2, fungu 19, mstari 9: Badili neno “kumbumbu” liwe “kumbukumbu.”
Ukurasa 187, safu 1, katika kisanduku, mstari wa 2: Badili maneno “vichwa viwili,” kuwa “pembe mbili.”
◼ Ili kusaidia katika matayarisho yenu ya kushiriki kikamili katika kuimba sifa za Yehova kwenye mkusanyiko wa wilaya, tuna furaha kutoa orodha ya nyimbo zitakazotumiwa wakati wa programu: Na. 19, 34, 172, 85, 136, 117, 121, 13, 155, 113, 105, 215, 174, 10, 53, 191, na 212. Kila familia inatiwa moyo kujizoeza kimbele nyimbo hizi kabla ya mkusanyiko ili kumsifu Mungu wetu kikamili zaidi kwa nyimbo.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana: Kiarabu: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani (Chapa ndogo).