Habari za Kitheokrasi
Ethiopia: Makusanyiko mawili ya mzunguko yalifanywa katika Addis Ababa katika Septemba kukiwa na hudhurio la pamoja la 5,842 na 201 wakabatizwa.
Japani: Ripoti yao ya mkusanyiko wa wilaya wa 1991 ilionyesha kilele cha hudhurio la watu 289,206, kukiwa na 4,851 wenye kubatizwa. Pia walifikia kilele kipya cha wahubiri 158,627 katika Julai, ongezeko la asilimia 11 kupita wastani wa mwaka jana.
Myanmar: Kujapokuwa mafuriko yenye maafa wakati wa Julai, walifikia kilele kipya cha wahubiri 1,810.
Ufilipino: Msaada wenye kuendelea unaandaliwa ili kusaidia waliopatwa na msiba wa mlipuko wa Mlima Pinatubo. Hivi karibuni, mvua nyingi na mitiririko ya matope, au lahars, ilifanyiza matatizo makubwa kwa akina ndugu ambao hawakuwa wamedhuriwa hapo mbeleni. Akina ndugu wanathamini msaada huo, kwa kuwa katika sehemu fulani hali zilikuwa mbaya zaidi katika Septemba kuliko wakati volkeno ilipolipuka hapo kwanza.
Tanzania: Jumla ya watu 189 walikuweko kwenye kuwekwa wakfu kwa Jumba la Ufalme la South katika Dar es Salaam Agosti 17.