Habari za Kitheokrasi
◆ Bolivia iliripoti kilele kipya cha wahubiri 6,701 katika Julai. Kijapokuwa kipupwe chenye baridi, wahubiri wa kundi walikuwa na wastani wa saa 14.2 katika utumishi.
◆ Côte d’Ivoire iliripoti kilele kipya cha wahubiri 3,070 mwezi Julai. Kulikuwako wahubiri 717 katika kazi ya painia, ikiwa ni asilimia 23 ya wahubiri. Mapainia wanaongoza asilimia 51 ya mafunzo ya Biblia.
◆ Ekwedori inaendelea kuona ukuzi mzuri. Kilele kipya cha wahubiri 15,201 katika Julai ni ongezeko la asilimia 20 juu ya wastani wa mwaka uliopita. Mapainia wasaidizi waliongezeka asilimia 66 juu ya mwezi uo huo wa mwaka jana.
◆ Mkusanyiko wa wilaya katika Guiana ya Kifaransa ulihudhuriwa na 1,425, na 28 walibatizwa. Walikuwa na kilele cha wahubiri 570.
◆ Guadeloupe iliripoti kwamba 12,339 walihudhuria mikusanyiko ya wilaya, na 308 walibatizwa. Ni vizuri sana ikilinganishwa na kilele chao cha wahubiri 5,980.
◆ New Zealand ilikuwa na ongezeko la asilimia 10 katika Julai wakiwa na kiele kipya cha wahubiri 11,007.
◆ Katika Agosti na Septemba jumla ya madarasa 16 ya Shule ya Painia yaliongozwa katika Afrika Mashariki yakifaidi wafunzi 278.
◆ Mfululizo wa makusanyiko ya mzunguko uliomalizika hivi karibuni ulikuwa na matokeo haya: Kenya: 10,626 walihudhuria na 130 wakabatizwa; Tanzania: 4,314 walihudhuria na 93 wakabatizwa; Uganda: 1,447 walihudhuria na 34 wakabatizwa.
◆ Ndugu na watu wenye kupendezwa zaidi ya 170 walihudhuria kuwekwa wakfu hivi karibuni kwa Jumba la Ufalme la Nyali, Mombasa.