Habari Za Kitheokrasi
Angola: Ongezeko zuri ajabu laendelea kuripotiwa. Kulikuwako kilele kipya cha wahubiri 18,911 katika Julai, na mafunzo ya Biblia 6,075 kuongozwa.
India: Jumla ya wahubiri walioripoti Julai ilikuwa 12,169, au asilimia 14 zaidi ya wastani wa mwaka jana. Mafunzo ya Biblia nyumbani yalifika kilele kipya cha 10,153.
Myanmar: Kilele kipya cha wahubiri 1,958 kilifikiwa katika Julai.
São Tomé na Príncipe: Kilele cha wakati wote cha wahubiri 80 walishiriki katika utumishi wa shambani katika Julai. Hesabu ya mafunzo ya Biblia yaliyoongozwa—382 katika Julai—inafunua kwamba eneo hilo kwa kweli liko tayari kwa mavuno mengi.