Habari Za Kitheokrasi
Côte d’Ivoire: Wahubiri walioripoti katika Juni walijumlika kuwa 4,330, kikiwa kilele chao cha sita cha wahubiri mwaka huu wa utumishi.
Italia: Kilele kingine katika wahubiri kiliripotiwa katika Juni kukiwa na 198,179 katika utumishi wa shambani. Makutaniko mapya 22 yalifanyizwa wakati wa mwezi huo.
Kamerun: Kilele kipya cha wahubiri 18,810 kilifikiwa katika Juni, na kulikuwa 84 waliobatizwa wakati wa mwezi huo.
São Tomé na Príncipe: Mnamo Juni 30 shirika moja lilianzishwa kihalali, likifungua mlango kwa ajili ya utendaji mwingi zaidi. Wahubiri 100 walioripoti katika mwezi huo wawakilisha ongezeko la asilimia 43 kupita wastani wa mwaka jana.
Uruguay: Kilele kipya cha wahubiri 9,093 kilifikiwa katika Juni.