Shule ya Huduma ya Ufalme Huandaa Elimu ya Kitheokrasi
Wazee huwa na daraka nzito. Kuanzia 1959, mipango ilifanywa kwa “mtaala wa mazoezi wa kipekee katika utendaji wa waangalizi” ili kuwasaidia washughulikie mgawo huu mzito. (jp kur. 292-3; yb77 kur. 14 Kiingereza) Watumishi wa huduma walialikwa kuhudhuria kwa mara ya kwanza katika 1984. Shule ya Huduma ya Ufalme ya mwisho ilifanywa wakati wa mwaka wa utumishi wa 1988, na makumi ya maelfu walifaidika.
Tangu wakati huo, mamia ya makundi yameundwa na maelfu ya akina ndugu wamewekwa kuwa wazee na watumishi wa huduma. Pia, marekebisho ya kitengenezo yamefanywa. Kwa hiyo, Baraza Linaloongoza lilipanga kwamba wazee wote wa kundi na watumishi wa huduma wahudhurie Shule ya Huduma ya Ufalme wakati wa mwaka huu wa utumishi. Habari kuhusu tarehe, mahali, n.k. itaandaliwa kwa wakati. Mtaala huo mpya umefanyizwa ili kukabiliana na mahitaji ya sasa shambani. Wawakilishi wa Betheli na baadhi ya waangalizi wasafirio wataongoza katika kufundisha kwenye shule hiyo. Faida zitapatikana kwa makundi yote wazee na watumishi wa huduma watumiapo yale wanayojifunza kutoka shule hiyo.