Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 16
  • Watumishi wa Huduma Wana Majukumu Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watumishi wa Huduma Wana Majukumu Gani?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Watumishi wa Huduma Hufanya Utumishi Muhimu
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Watumishi wa Huduma Ni Baraka kwa Watu wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Watumishi wa Huduma Dumisheni Msimamo Mzuri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Kudumisha Upatano Kati ya Wazee na Watumishi wa Huduma
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 16

SOMO LA 16

Watumishi wa Huduma Wana Majukumu Gani?

Mtumishi wa huduma akisaidia kugawa machapisho

Myanmar

Mtumishi wa huduma akitoa hotuba

Mkutano

Mtumishi wa huduma akiongoza mkutano

Kikundi cha utumishi

Mtumishi wa huduma akifanya usafi katika Jumba la Ufalme

Udumishaji wa Jumba la Ufalme

Biblia hutaja vikundi viwili vya wanaume Wakristo ambao hushughulikia majukumu ya kutaniko, yaani, “waangalizi na watumishi wa huduma.” (Wafilipi 1:1) Kwa kawaida, katika kila kutaniko kuna wazee na watumishi wa huduma kadhaa. Watumishi wa huduma wanafanya kazi gani kwa faida yetu?

Wanalisaidia baraza la wazee kutanikoni. Watumishi wa huduma ni wanaume wa kiroho, wenye kutegemeka, na wenye bidii. Baadhi yao ni vijana na wengine wana umri mkubwa. Wanafanya kazi za kawaida lakini ambazo ni muhimu kutanikoni. Utumishi wao huwawezesha wazee kupata wakati wa kukazia fikira ufundishaji na uchungaji.

Wanatimiza huduma muhimu. Baadhi ya watumishi wa huduma hupewa mgawo wa kuwakaribisha wote wanaofika mikutanoni. Wengine hushughulikia mfumo wa sauti, vitabu na magazeti, hesabu za kutaniko, na migawo ya maeneo kutanikoni. Pia, wao husaidia katika kudumisha Jumba la Ufalme. Wazee wanaweza kuwaomba wawasaidie ndugu na dada waliozeeka. Hata iwe wana migawo gani, wanastahili kuheshimiwa na wote kutanikoni kwa sababu ya roho yao ya kutumikia.—1 Timotheo 3:13.

Wanaweka mfano mzuri. Watumishi wa huduma huwekwa rasmi kwa sababu ya sifa zao nzuri za kiroho. Wanaposhughulikia migawo yao katika mikutano, wanaimarisha imani yetu. Wanapoongoza katika kazi ya kuhubiri, wanatuchochea kuwa wenye bidii. Roho yao ya ushirikiano huchangia shangwe na umoja. (Waefeso 4:16) Baada ya muda, huenda wao pia wakastahili kutumikia wakiwa wazee.

  • Watumishi wa huduma ni watu wa aina gani?

  • Watumishi wa huduma wanalisaidiaje kutaniko?

PATA KUJUA MENGI ZAIDI

Kila mara unapokwenda kwenye Jumba la Ufalme, jitahidi kumfahamu angalau mmoja wa wazee au watumishi wa huduma mpaka utakapowajua wote pamoja na familia zao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki