Habari Za Kitheokrasi
Korea: Kilele kipya cha wahubiri 68,310 kilifikiwa katika Januari. Makundi saba yaliripoti kwamba wahubiri wote waliobatizwa walishiriki katika aina fulani ya utumishi wa wakati wote. Kundi moja liliripoti mapainia wa kawaida 12, mapainia wasaidizi 15, na hakukuwa na wahubiri wa kundi.
Naijeria: Ripoti ya Januari ilionyesha kilele kipya cha wahubiri 156,001, ongezeko la asilimia 7 kupita wastani wa mwaka jana.