Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti
Juma Linaloanza Agosti 3
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Onyesha mambo ya kuzungumzia katika magazeti ya karibuni. Watie moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani mwishoni mwa juma hili.
Dak. 15: “Matangulizi ya Kuchochea Kupendezwa.” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Toa wonyesho wa mambo yaliyo katika fungu la 5.
Dak. 20: “Hatua Zifaazo Ili Kufanya Maendeleo Zaidi.” Toa mafungu ya kwanza mawili ya nyongeza kwa njia ya hotuba. Pitia makala inayobaki kwa maswali na majibu. Kazia mambo yanayoweza kutumiwa kwenu. Malizia kwa muhtasari mfupi.
Wimbo 155 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu, kutia na ripoti ya hesabu na shukrani kwa upaji. Pongeza kundi kwa utegemezo wa kifedha kwa kundi lenu, na kwa kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote.
Dak. 20: Kusitawisha Kupendezwa Katika Ziara za Kurudia. Mazungumzo na mwangalizi wa utumishi. Wengi huliona kuwa jambo la kufurahisha kuzungumza na watu na kuacha fasihi. (om-SW kur. 87-8) Daraka letu linatia ndani kusitawisha kupendezwa katika mioyo ya wale tunaozungumza nao. Toa wonyesho mfupi kuonyesha jinsi trakti inavyoweza kutumiwa kusitawisha kupendezwa katika ziara ya kurudia mahali ambapo fasihi haikuangushwa kimbele. Kazia jambo moja au mawili tu. Toa wonyesho mfupi kuonyesha jinsi habari zinazopatikana katika faharisi ya kitabu Kutoa Sababu zinavyoweza kutumiwa. Kazia mambo machache na ya waziwazi yaliyo katika kichapo yanayoweza kutumiwa kusitawisha kupendezwa katika Biblia. Onyesha jinsi ya kupanga kwa ajili ya ziara nyinginezo zaidi.
Dak. 15: “Babuloni Mkuu.” Mazungumzo juu ya kitabu Kutoa Sababu, kurasa 35-9. Wonyesho: Mhubiri azungumza na mwanafunzi wa Biblia juu ya maendeleo yake. Akazia uhitaji wa kuonwa na Yehova kuwa watakatifu, kuwa tunastahili msaada na baraka Zake. (1 Pet. 1:15, 16) Kazia umaana wa kukimbia kutoka Babuloni sasa na kushirikiana na tengenezo takatifu la Yehova. Mwenyekiti amalizia kwa kuwatia moyo akina ndugu watumie vichapo ili kuelekeza wanafunzi kwenye tengenezo na kutumia vizuri msaada ambao wazee wanatoa.
Wimbo 129 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 17
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Watie moyo akina ndugu wafanye mipango ya mapema kwa ajili ya mikutano na kushiriki kikamili. (Ebr. 10:23-25) Pia, tia moyo ushiriki katika utendaji wa shambani mwishoni mwa juma.
Dak. 20: “Takwa la Kufanya Ziara za Kurudia.” Maswali na majibu. Baada ya kuzungumzia fungu la 5 na 6, uwe na maonyesho mawili. (1) Onyesha jinsi trakti inavyoweza kutumiwa ili kuanzisha funzo la Biblia. (2) Teua habari fulani katika kitabu Kutoa Sababu na uonyeshe jinsi inavyoweza kutumiwa kujibu swali kwenye ziara ya kurudia. Kazia thamani ya vipindi vya mazoezi. Tia moyo kufuatia wote wanaopendezwa.
Dak. 10: Mazungumzo juu ya makala “Je! Wakumbuka?” katika Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1992. Tia moyo wote wadumishe ratiba nzuri ya kusoma magazeti. Toa madokezo yanayotumika.
Wimbo 130 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 24
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Kufanya Kazi kwa Njia Yenye Matokeo Nyumba kwa Nyumba.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Tia moyo kufanya upainia msaidizi katika Septemba. Taja kwamba wale wanaofanya upainia msaidizi mara nyingi hudumisha kiwango cha juu cha utendaji katika miezi inayofuata.
Dak. 15: Peleka Watoto Wako Shuleni Wakiwa na Mawazo ya Mungu Ndani ya Mioyo Yao. Hotuba ikitolewa na mzee. Tunaishi katika ulimwengu wenye mwelekeo wa kujaribu kutufinyanga katika mfinyango wao. Na hilo ni kweli hasa kwa vijana wetu. Wazazi wanahitaji kuona haraka mahitaji na matatizo yao. (Mit. 20:5) Kaza akilini mwao sheria za Mungu na upendo wake pamoja na upendo wa wazazi. Wonyesho: Familia yazungumzia jinsi ya kutumia broshua Shule. Mtoto mmoja anaenda shule kwa mara ya kwanza, hali wale wengine wawili wamekuwa wakienda shule kwa miaka kadhaa. Teua jambo litakalotumika katika hali za kila mmoja wao. Watoto waeleze kwa maneno yao wenyewe wakimwambia mzazi anayeigiza sehemu ya mwalimu. Hakikisha watoto wanaelewa kanuni zinazohusika. Ndugu anayeshughulikia sehemu hiyo atia moyo kuwe na funzo la Biblia la familia na akazia uhitaji wa wazazi kuwa na uhusiano wa karibu, wa kuhisiwa moyoni na watoto wao.
Dak. 10: “Kutumia Kitabu Kuishi Milele Katika Ziara za Kurudia” Kwa ufupi, zungumzia habari katika mafungu mawili ya kwanza. Halafu toa wonyesho wa ziara ya kurudia kwa kutumia maneno ya utangulizi wa moja kwa moja ili kuanzisha funzo la Biblia.
Wimbo 126 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 31
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: Je! Wewe Unafanya Maendeleo ya Kiroho? Mazungumzo na mzee. Je! wale walio kundini wametimiza miradi hususa katika mwaka wa utumishi uliopita? Ikiwa sivyo, kwa nini? Dokeza miradi fulani. Maendeleo yanahitajiwa ili kutunza hali ya kiroho. (Flp. 3:16) Wonyesho mfupi wa familia, wakati wa funzo la familia, wakipitia huduma yao wenyewe kuona ni wapi wanapoweza kufanya maendeleo ya kiroho.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu au mazungumzo ya utendaji wa utumishi wa shambani wa kundi yakifanywa na mzee.
Dak. 15: Toa kitabu Creation katika Septemba. (Mahali ambako kichapo hiki hakipatikani katika Kiswahili, tumia habari hii na wonyesho uhusu ama kitabu Kuishi Milele ama Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia.) Hotuba pamoja na wonyesho. Zungumzia habari ya kukaziwa na vielezi vinavyoweza kuonyeshwa tunapotoa kitabu Creation. Habari katika kitabu Kutoa Sababu chini ya kichwa “Uumbaji” yaweza kutumiwa mahali inapowezekana. Labda habari katika sura 16 na 19 juu ya “Kwa Nini Mungu Angeweza Kuruhusu Kuteseka?” na “Paradiso ya Kidunia Inayokuja Karibuni” yaweza kumvutia mwenye nyumba. Mhubiri anayestahili atoe wonyesho wa toleo, akitumia Mithali 2:21, 22 na picha kwenye ukurasa 197, akikazia kwamba kusudi la Mungu la kwanza la kuumba dunia litatimizwa karibuni.
Wimbo 109 na sala ya kumalizia.