Msifu Mungu wa Uumbaji
1 Sura za nchi zenye kupendeza, machweo yenye kuvutia, anga la usiku lenye nyota, nyimbo tamu za ndege—wewe unamsifu nani kwa ajili ya mambo hayo yenye kupendeza? Naam, sisi tunasukumwa kumsifu Mungu wa uumbaji. Tunakubaliana kwa moyo wote na julisho rasmi kwenye Ufunuo 4:11. Yehova Mungu astahili sifa yetu kwa maana ni yeye aliyeumba vitu vyote.
2 Kujapokuwa na uthibitisho wa kazi za Mungu za uumbaji, wanadamu wameendeleza wazo la kwamba uhai ulianza kwa aksidenti au kwa mageuzi yasiyo na mwongozo. Uwongo huo mkuu umewashusha na kuwavunja moyo wanadamu, na ni suto lenye kumkufuru Muumba wetu Mtukufu—Mhu. 12:1; Rum. 1:20, 25.
3 Katika Septemba, tuna fursa ya kutoa kweli kuhusu Muumba wetu na kazi zake za ajabu, tukiwa watumishi waaminifu-washikamanifu wa Yehova. Kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? kitatolewa kwa wote wanaoonyesha kupendezwa kikweli kujifunza mambo hakika kuhusu asili na kusudi la uhai. Kichapo hicho kinatutayarisha tutetee kwa ujasiri ile kweli kuhusu asili ya uhai.
4 Maeneo ya Pekee: Licha ya kutoa ushahidi nyumba kwa nyumba, tunaweza kufanya jitihada ya pekee kuzungumza na watu wanaopendezwa kihususa na habari ya mageuzi au uumbaji, tukiwafikia ama kazini mwao ama shuleni. Kwa mfano, Mashahidi wachanga wamekuwa na matokeo mazuri katika kuangusha kitabu Creation wanapokionyesha kwa walimu wao. Kijana mmoja Shahidi alimpa mwalimu wake kitabu Creation akashangaa kuona kwamba mwalimu huyo hakukisoma tu kikamili bali pia alianza kukitumia kuwa msingi wa kufunzia darasa. (w90-SW 9/1 uku. 32; w86-SW 10/1 uku. 32) Kwa nini usimfikie kila mmoja wa walimu wako na wanadarasa wenzako ambao unahisi wangefurahia kusoma kichapo hicho kizuri.
5 Jitihada ya pekee inaweza kufanywa ya kuwafikia wanafunzi na wafunzi wa vyuo wanaoishi au kufanya kazi katika eneo lenu. Watu wenye stadi za kazi kama vile mawakili na madaktari wamethamini kina cha utafiti na habari zinazopatikana katika kitabu Creation. (yb87-E uku. 54) Huenda wale unaofikia wakataka pia kupata kichapo hicho chenye vielezi vyenye kupendeza kikiwa kitabu cha marejezo.
6 Kifaa hiki kizuri na kiwasaidie watu wengi zaidi waone jinsi nadharia ya mageuzi isivyo ya akili na pia kiwasaidie kujenga uthamini wao kwa zawadi ya uhai. Kitabu hiki kitachochea ndani yao tamaa ya kuishi milele kwa utukufu wa Mpaji uhai na ‘Mfanyi wa mbingu na nchi.’—Zab. 146:6.