Utoaji Mbalimbali Ulio Rahisi na Wenye Matokeo
1 Yesu alipiga mbiu ya Ufalme wa Mungu katika njia rahisi ya moja kwa moja. Alijua kwamba watu wenye mfano wa kondoo wangeitikia ifaavyo wakati wangeisikia kweli. Pia alijua kwamba watu hutofautiana katika kufikiri, mapendezi, na uwezo wao wa kutoa sababu. Kwa hiyo, alitumia tangulizi mbalimbali, maswali, na vielezi rahisi ili kunasa uangalifu wa wasikilizaji wake na kugusa mioyo yao. Tunaweza kuiga mfano wake na kutumia ifaavyo utoaji mbalimbali ulio rahisi na wenye matokeo.
2 Tumia Kitabu Kutoa Sababu kwa Matokeo: Utangulizi wa kwanza chini ya kichwa “Kazi ya Kuajiriwa/Nyumba” kwenye ukurasa 11 wa kitabu Kutoa Sababu ni wa wakati ufaao na ni rahisi kutoa.
Unaweza kusema:
◼ “Tumekuwa tukizungumza na majirani wako kuhusu yale yanayoweza kufanywa ili kuhakikisha kwamba kutakuwa na kazi ya kuajiriwa na nyumba kwa kila mtu. Je! unaamini kwamba ni jambo la akili kutarajia kwamba siku moja tatizo hilo litasuluhishwa? . . . Lakini kuna mtu anayejua jinsi ya kusuluhisha matatizo hayo; huyo ni Muumba wa ainabinadamu.” Soma Isaya 65:21-23. Kisha unaweza kumuuliza mwenye nyumba maoni yake juu ya hilo.
3 Utangulizi chini ya kichwa “Udhalimu/Kuteseka” kwenye ukurasa 12 utavutia wengi leo.
Unaweza kuuliza:
◼ “Je! Umepata kujiuliza: Kweli Mungu hujali kuhusu udhalimu na kuteseka ambako binadamu hupata?” Ruhusu mwenye nyumba ajibu na kisha usome Mhubiri 4:1 na Zaburi 72:12-14. Ikiwa inafaa kuonyesha kitabu Kuishi Milele, fungua kwenye picha katika kurasa 150-3 na uonyeshe kifupi jinsi hali za ulimwengu leo zinatimiza unabii wa Biblia. Kisha fungua kurasa 161-2 kuonyesha yale ambayo Mungu ametabiri zaidi kwa ajili ya baraka za mwanadamu. Muulize mwenye nyumba ni jambo gani lamvutia zaidi ya yote.
4 Baada ya mazungumzo mafupi na mwenye nyumba, huenda ukaamua kwamba itafaa zaidi kuelekeza fikira zake kwenye makala katika mojawapo magazeti, kwa broshua, au kwa trakti kuliko kwa kitabu Kuishi Milele.
Kwa mfano, baada ya kutumia utangulizi ulio katika fungu 2 la makala hii, huenda ukasema:
◼ “Broshua hii, Je! Kweli Mungu Anatujali?, hueleza waziwazi yale ambayo Mungu ameahidi kufanya ili kushughulikia mahitaji yetu ya kila siku na huonyesha jinsi sisi tunavyoweza kunufaika.” Fungua kurasa 26 na 27 za broshua, na uelekeze fikira kwenye fungu 21.
5 Au baada ya kutumia utangulizi katika fungu 3, trakti Je! Ulimwengu Huu Utaokoka? yaweza kukaziwa.
Unaweza kusema:
◼ “Kuna taabu na matatizo mengi ulimwenguni leo. Trakti hii inaonyesha kwamba vita, upungufu wa chakula, na matatizo ya afya yalitabiriwa yote katika Biblia. Lakini Mungu ameahidi pia kuleta badiliko zuri ajabu kwa ainabinadamu.” Soma fungu la mwisho kwenye ukurasa 5 wa trakti.
6 Kupendezwa kwetu na watu kwa unyofu, pamoja na utoaji ulio rahisi na wenye matokeo unaogusa moyo, kwa kweli utawavutia wenye mfano wa kondoo.—Yn. 10:16.