Je! Wewe Unatumia Utangulizi Unaofaa?
1 Mwenye nyumba anapofungua mlango, mhubiri wa habari njema anakabili mwito wa ushindani wa kutoa ujumbe wa Ufalme katika njia inayofaa. Katika muda mchache unaofuata, mara nyingi mwenye nyumba ataamua ikiwa atasikiliza utoaji huo au atamfukuza huyo Shahidi. Tukiwa wahubiri wa Ufalme, tunajua kwamba habari tunayopeleka ni ya maana sana, na kwa kweli tunataka kusaidia wale tunaozungumza pamoja nao. (Rum. 10:14) Lakini tutakuwa na fursa ya kushiriki kweli za Biblia tunazopeleka ikiwa utangulizi wetu unavutia fikira ya mtu huyo.—Kol. 4:6; linganisha Mithali 25:11.
2 Katika kufikiria kufaa kwa utangulizi wetu, lingekuwa jambo zuri kujiuliza wenyewe ikiwa tumeanguka katika mtego wa kutumia utangulizi ule ule kwa kurudia-rudia kwa sababu ni rahisi kuukumbuka au tunahisi tumestarehe kuutumia. Je! kuna maneno fulani katika utangulizi wetu ambayo yanaweza kutokeza maoni ya ubaguzi katika maeneo fulani? Je! ni mahususi vya kutosha kuamsha kupendezwa tangu mwanzo, au unaruhusu mwenye nyumba kukatisha mazungumzo hata kabla hatujaingia katika habari yetu? Ni jinsi gani tunaweza kuamsha kupendezwa kwa mwenye nyumba mapema katika mazungumzo yetu? Matangulizi yenye matokeo hayatokei hivi hivi tu. Yanahitaji kazi nyingi, kutayarisha kwa umakini na kufanya mazoezi kwa ukawaida.
KUCHAGUA UTANGULIZI UNAOFAA
3 Kuanzia ukurasa 9 wa kitabu Reasoning, kuna kisehemu bora sana chenye kichwa “Matangulizi ya Kutumia Katika Huduma ya Shambani.” Pitio la maelezo yanayofungua kisehemu hicho bila shaka litakuwa lenye msaada sana. Mwanzoni kabisa, tunakumbushwa kwamba tunahitaji makaribio tofauti kwa maeneo tofauti, watu, na mastakimu. Uteuzi wa utangulizi unaofaa unahitaji ufikirio wa umakini.
4 Unapotoa ujumbe wa Ufalme, je! unaweza kuonyesha jinsi utanufaisha mwenye nyumba kibinafsi? Kama kielelezo, fikiria utangulizi wa kwanza chini ya kichwa “Uhalifu/Usalama” kwenye ukurasa 10 wa kitabu Reasoning. Katika taarifa ya kwanza, habari yenye umuhimu kwa mwenye nyumba inatangulizwa. Mazungumzo yanayofuata yangeonyesha daraka la Ufalme katika kumaliza uhalifu.
5 Ni jinsi gani tunaweza kuondosha vipingamizi vinavyozuia mwenye nyumba asitake kufikiria ujumbe wetu? Vichwa vilivyo kwenye kurasa 14 na 15 katika kitabu Reasoning vinatoa madokezo bora. Mathalani, fikiria jinsi unavyoweza kutumia utangulizi ulio chini ya kichwa “Watu Wengi Wanaposema: ‘Mimi Nina Dini Yangu Mwenyewe.’” Taarifa ya kwanza yaweza kuamsha kupendezwa kwa mwenye nyumba. Je! unaweza kutumia utangulizi huu katika eneo lako?
6 Tunaweza kuonyesha kupendezwa kwetu kikweli katika hali ya mwenye nyumba jinsi gani? (Marko 6:34) Tabasamu ya moyo mweupe, na ya urafiki inaweza kusaidia. Urafiki unavutia wengine na unalingana na kusudi letu la kusaidia watu. Kupendezwa kwetu na mwenye nyumba kunaonyeshwa pia kwa kumtia moyo atoe maelezo yake. Kuomba maoni yake kwa unyoofu kunaweza kumsaidia sana asikilize ujumbe wetu. Kielelezo cha jambo hili kinaonekana katika utangulizi wa pili chini ya “Ufalme” kwenye ukurasa 12. Je! wewe umetumia huo? Kwa kawaida, watu wanapenda kutoa maoni yao, nao wana udadisi ni maswali gani utauliza. Ingawaje, tukitaka kuendeleza kupendezwa kwao, lazima tusikilize itikio lao kisha turekebishe utoaji wetu ili kutumia kwa faida yale ambayo tumejifunza kutokana na rai zao.
KUWA MACHO KUONA MASTAKIMU
7 Unapokaribia mlango, tazama mazingira. Je! kuna vitu vya kuchezea katika ua, nguo zimeanikwa, vitu vya kidini mlangoni, na kadhalika? Mwenye nyumba anapokuja mlangoni, tunaamkuliwa na mwanamume au mwanamke, kijana au mzee, mama, baba, au mtoto? Uhakika wote huu unaweza kutusaidia tuchague utangulizi unaofaa uliotayarishwa vizuri kulingana na hali na mapendezi ya mtu anayetuamkua.
8 Matangulizi yanayodokezwa katika kitabu Reasoning yamejaribiwa yote, na yamethibitika kuwa yenye mafanikio. Mbona usijitahidi kuyatumia katika eneo lako? Angalia ni yapi yenye matokeo zaidi. Yaelekea utapata kwamba kwa kutayarisha vizuri, kutia ndani vipindi vya kawaida vya kufanya mazoezi, matangulizi yako yatakuwa yenye matokeo zaidi na utakuwa na mafanikio zaidi katika kueneza Neno la uhai.—Mt. 13:18-23.